Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali yangu kwa kazi nzuri sana ya maendeleo ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo kubwa Musoma Mjini kwani wananchi waliombwa kupisha eneo la Jeshi katika eneo la Makoko na wameendelea kupata ahadi ya kulipwa fidia. Sasa ni zaidi ya miaka kumi hadi leo bado hawajapata chochote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anakumbuka wale wananchi walituma mwakilishi wao. Na mimi nilimleta kwake na tukakaa pamoja akaahidi kwamba katika bajeti hii hao wananchi wa Musoma watalipwa fidia. Naomba kauli yake hapa Bungeni, kwani wamehangaika kwa muda mrefu sana ili suala hilo tulimalize.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja ya bajeti ya Wizara hii.