Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya yote ninaunga mkono hoja kwa asilimia zote. Napenda kuwapongeza Waziri na Katibu Mkuu wake kwa kusimamia, kuiongoza na ufuatiliaji wao wa karibu zaidi wa majukumu ya Wizara yao, pamoja na changamoto zote na ukosefu wa kupatiwa bajeti katika ukamilifu wake kama ilivyopitishwa na Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikizungumza kwa uchungu kuhusu Mkoa wetu, hapo awali tulikuwa na makambi ya JKT Milundikwa na Luwa, Rukwa ambayo yalitusaidia kuwaweka vijana wetu ndani ya maadili ya uzalendo na ulinzi uliotukuka wa ushirikishwaji na wananchi wetu, sasa kama itakuwa Serikali (Hazina) haitoi fedha za kukidhi mahitaji kwa angalau asilimia 75 kwa umuhimu wa Wizara hii, kwani hawana masaa maalum ya utumishi wao, hivyo kuna umuhimu wa kupewa fedha za maendeleo kwa asilimia hiyo ili makambi haya yakarabatiwe na kuanza kutumika mapema, kwani vijana wanaongezeka mitaani/Vijijini baada ya kumaliza masomo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016/2017 zimetolewa fedha za maendeleo shilingi 35,900,000,0000 ikiwa ni asilimia 14.5 ya bajeti iliyoidhinishwa mwaka 2017/2018. Bajeti imepungua kwa shilingi 29,000,000,000 kwa bajeti ya mwaka 2016/2018 iliyokuwa shilingi 248,000,000,000 na sasa kuwa 219,000,000,000 kwa mwaka 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba fedha za maendeleo ni vema zikatolewa kwa wakati na katika ukamilifu wake, kutokana na umuhimu wa:-

(i) Kukamilisha ukarabati wa makambi ndani ya mwaka 2017/2018, kuchelewa zaidi kutatuathiri.

(ii) Tuondokane na migogoro ya wananchi waliochukuliwa maeneo yao kwa matumizi ya Jeshi, walipwe fidia zao waweze kujiendeleza. Hizo bilioni 27 ni muhimu kwa sasa kabla ya Juni, 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madhumuni ya kukamilisha makambi ni kuwajenga vijana wetu kiuzalendo, kiulinzi na naishauri Serikali inapohitaji kuajiri Polisi, Wanajeshi, Maafisa Usalama wa Taifa, Uhamiaji, Jeshi la Zimamoto na Magereza usaili ufanyike kwa vijana waliopitia JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa vijana wanaopitia JKT baadhi wanabaki mitaani/vijijini ni bora vijana hawa wakaunganishwa kwenye huduma za ulinzi za SUMA Guard badala ya kurudi kujiunga na jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.