Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuchukua fursa hii kumshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa kuwasilisha hotuba vizuri juu ya maendeleo na utekelezaji kwa ujumla wa Wizara. Vilevile niwapongeze kwa dhati watumishi wote wa Wizara kwa kazi nzuri ya ulinzi wa Taifa letu. Hii imewezesha kuwepo kwa hali ya utulivu na amani ya nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishukuru Wizara kwa mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa vijana wetu kwani wanapata maarifa na ujuzi hasa katika stadi za kazi zinazowawezesha kujiajiri na kujitegemea. Hivyo, ninaomba na kuishauri Serikali kuongeza idadi ya vijana wa kujiunga na JKT kutoka 20,000 hadi 25,000 kwa mwaka 2017/2018, hii itasaidia vijana wengi zaidi kujishughulisha kutokana na ujuzi wanaoupata kutokana na mafunzo ya JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo muhimu ninalopenda kuwasilisha ni juu ya wapiganaji vita vya Kagera. Wapo wanajeshi wengi nchini Tanzania wanadai mafao yao. Mwaka jana niliuliza juu ya suala hili na katika maelezo ya wanajeshi hawa ni kwamba Serikali Awamu ya Nne ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete waliahidiwa kulipwa mafao yao, mpaka sasa hakuna chochote. Nimeangalia kwenye bajeti iliyowasilishwa ya mwaka 2017/2018 sijaona kabisa kuzungumziwa suala hili. Ninaomba Mheshimiwa Waziri, nipate maelezo ya kina juu ya suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimelileta suala hili kutokana na wanajeshi walioko Jimboni kwangu Busanda wamekuwa wakifuatilia sana juu ya suala hili, ninaomba nipate maelezo ya kina na ufafanuzi juu ya suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo haya, naunga mkono hoja.