Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nashukuru sana kupata nafasi hii ili niweze kuchangia Hotuba ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yake wameandaa hotuba nzuri sana ambayo nadhani imetupa changamoto ya kuijadili hapa ndani. Vilevile ningependa nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, yeye ana jina lake ambalo kule mtaani katika vile viunga vya viwanda tunamuita mzee wa sound, halafu anasema kwamba yeye mke wake anamwita ni handsome boy. Kazi yake ni nzuri sana Mheshimiwa handsome boy, Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ningependa kuzungumzia masuala makuu matatu. La kwanza, kuna haja kubwa sana sasa ya kujaribu kuoanisha vizuri sana kazi anayofanya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na kazi ambayo Mheshimiwa Waziri wa Fedha anaifanya, kwa sababu pale ndipo tunapoanzia kutofautiana. Mheshimiwa Waziri wa Viwanda anafanya kazi kubwa sana ya kupiga debe na kuhakikisha hii philosophy ya uchumi wa viwanda inaanza kwa kasi sana hapa nchini, lakini bado kuna hiccup kubwa sana upande wa Wizara ya Fedha; kwa sababu huyu ataweza tu kuwa na philosophy ya uchumi wa viwanda kama na mambo yote yanayohusu mambo ya kodi na vivutio kwa wawekezaji yanakwenda samabamba. Vinginevyo itakuwa ni wimbo ambao utaendelea kuimbwa na hatutapata majibu ya haraka haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nimuombe Mheshimiwa Waziri atoe tafsiri zaidi anaposema viwanda, kwa sababu tumekuwa tukichangia hapa tunasema mimi kwangu hakuna kiwanda, viwanda vimesimama sijui magunia na kadhalika. Tafsiri ya kiwanda kutoka kwa industrial economist ni kitu chochote ambacho kinaweza ku- transform bidhaa moja kwenda kuwa bidhaa nyingine inayoweza kutumika. Kama ni mbao kuwa kitu au meza na kadhalika, kama ni kuchanganya dawa basi iweze kutumika kama dawa na kadhalika, from chemicals to drugs.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo katika hali ya kawaida bado tunapata ukakasi kwamba ni namna gani tunazungumzia dhima nzima ya uchumi wa viwanda. Ukiangalia Serikali inajaribu kuweka miundombinu na mazingira ya kumfanya mfanyabiashara au biashara iweze kufanyika hapa nchini.

Kwa mujibu wa takwimu za Benki Kuu kwa miaka mitano iliyopita, Tanzania tumeweza ku-export nje, India bidhaa zenye thamani ya dola bilioni 1.12, Kenya dola milioni 793, South Africa dola milioni 698, China dola milioni 620, Japan dola milioni 370. Lakini tumeweza ku-import, Saudi Arabia peke yake ni bidhaa za zaidi ya shilingi bilioni 5.6, China shilingi bilioni 2.23, India shilingi bilioni 1.24, Uarabuni shilingi milioni 789 na South Africa shilingi milioni 567. Kwa hiyo, ukiangalia Tanzania tumeweza ku-export lakini tumeingiza zaidi na hii ndiyo changamoto ambayo inaanzia pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia katika sura nzima, maeneo ya msingi lazima tuangalie namna ya kuweza kuongeza uwekezaji utakaoondoa ukiritimba wote na kuongeza ajira na tija kwa Watanzania, bila kufanya hivyo tutaimba wimbo huu hatutafanikiwa kuufikia. Hii nasema kwa sababu kumekuwa na tatizo kubwa sana sasa hivi hasa la wawekezaji. Wenzangu wamesema, nisingependa kurudia kwamba nchi yetu lazima tuweke utaratibu utakaoweza kuwa rafiki kwa wawekezaji kuwekeza hapa nchini. Mtu hawezi kuwekeza hapa nchini kama kuna uncertainties na unpredictable tax regimes, haiwezekani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi ninachoomba sana katika hili tumsaidie Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, si la kwake peke yake; na Bunge hili tuna jukumu la kuishauri Serikali yetu, kwamba ni namna gani masuala haya yanaweza kuoanishwa na kuhuishwa kwa ajili ya kuchochea uwekezaji hapa nchini. Sisi si kisiwa, Tanzania tuna vivutio vingi sana, tuna maeneo mengi sana ya kuwekeza lakini sisi na wenzetu tuna-compete hivyo lazima tuweke mazingira ambayo yatajenga assurance kwa mwekezaji anapokuja hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tutambue uwepo na ushiriki kamilifu wa sekta binafsi, hili ni suala la msingi sana. Najua tumekuwa na kasumba kwanza kutokutaka kuipenda private sector, lakini Waheshimiwa Wabunge, bila kuipenda private sector na kuipa nafasi ya ushiriki vizuri hatutaweza kutoka hapa tulipo. Acha Serikali iwekeze pale ambapo panatakiwa huduma itolewe na pengine pasipo faida, lakini maeneo ambayo yanahitaji kupata faida tuwekeze zaidi kwa hawa wawekezaji binafsi na tuingie utaratibu wa PPP, huu utasaidia kuipunguzia Serikali mzigo wa kutumia fedha zake katika kuwekeza na matokeo yake tuisaidie private sector iweze kuwekeza zaidi, Serikali inachotakiwa pale ni kuvuna kodi. Mimi naomba sana hili tuweze kuliangalia.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tuangalie mustakabali mzima kwamba Watanzania tunatoka hapa tulipo namna gani, uwekezaji huu unakuwa na tija gani kwa Mtanzania, lazima tupate tija ya uwekezaji huu katika huduma za afya, elimu na kadhalika. Hata hivyo tatizo lililopo sasa hivi ni mitaji, liquidity sasa hivi kwenye economy imekuwa so tight, lending rates zimekuwa kubwa, watu wanashindwa kukopa fedha na kuwekeza. Njia pekee ni ku-attract mitaji kutoka nje ili kusaidia kuwekeza hapa nchini lakini tutafanya vile kama wawekezaji hawa tutawawekea mazingira mazuri ya wao kuwekeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa na hadithi ya Mchuchuma na Liganga miaka nenda-rudi. Mheshimiwa Waziri, hebu tusaidie, pale ambapo unadhani kabisa kwamba inakushinda naomba Bunge hili likusaidie ili utusaidie tutoke hapa tulipo tuache kuimba nyimbo na ngonjera za kila wakati. Ukiangalia ufanyaji biashara hapa Tanzania kila kukicha unakuwa ghali zaidi. Kwenye sekta ya utalii peke yake kuna kodi zaidi ya 36, hivi kweli mtu atawekeza kwa kodi hizi 36? Haiwezekani! Mimi sitaki kuzisoma, ni nyingi sana. Kitu ambacho ninaomba sana Serikali yetu ijaribu kuwa sikivu, na hasa Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge lililopita niliwahi kusema Mheshimiwa Waziri wa Fedha atusaidie na kusaidia maana yake ni kwamba ajaribu kuwa kiungo na si mtenganishi wa masuala ya uchumi katika nchi. Nina imani kabisa kwamba Watanzania kama tutafuata msingi mzuri wa uwekezaji, tutasonga mbele. Dhima na dhana aliyonayo Mheshimiwa Waziri wa Viwanda ni nzuri, tunamsikia kila mahali anazunguka, hata ukikutana naye ukamwambia Mheshimiwa nataka kiwanda, anakwambia ntakupa kiwanda, anakupa hata matumaini hata kama hana, hiyo inatosha Mheshimiwa Waziri, unatupa matumaini. Hata hivyo ninaomba utuambie hapa vizuri zaidi tafsiri ya viwanda ili tuweze kuelewa kwa sababu unapotuambia viwanda tunawaza viwanda vikubwa tu. Kuna viwanda vidogo, vya kati na vikubwa, lakini kunakuwa na linkage ambayo inakuwepo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tunasifika kwa kuwa na uchumi unaokuwa pamoja na sera nzuri au tulivu za uchumi. Hizi lazima ziwe translated katika mahitaji ya Watanzania. Level ya umaskini Tanzania bado ipo katika kiwango cha juu na ndiyo maana hata Mheshimiwa Rais anasema sitaki kuona wananchi masikini wanateseka, he is for the poors, lakini sisi tunafanya nini kusaidia kauli mbiu hii.

Mheshimiwa Rais amejitahidi sana na kwa muda mfupi tunaweza kuona kwamba nchi sasa inaanza kusonga mbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeanzisha na miradi ambayo ni mikubwa yenye kusimika uchumi wa nchi, kwa sababu bila kuwa na logistics and division systems huwezi ukapanua nchi yako. Lakini sisi kama Tanzania, leo ujenzi wa reli ni mardi mkubwa sana, unahitaji gharama kubwa sana lakini pindi utakapokwisha utakuwa ni uti wa mgongo wa uchumi wa nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuunga mkono hotuba hii, ahsante sana.