Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishauri Serikali mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imepania kuwa na Tanzania ya viwanda, naiomba Serikali ianzishe au itafute wawekezaji kwa ajili ya Mkoa wa Njombe. Njombe ni katika mikoa inayozalisha kwa wingi chakula kama vile mahindi, ngano, alizeti na matunda. Hivyo, naiomba Serikali itafute wawekezaji kwa ajili ya kiwanda cha kusindika matunda, unga wa mahindi na unga wa ngano Mkoani Njombe. Pia naiomba Serikali ianzishe au itafute wawekezaji kwa ajili ya viwanda vya karatasi, lami, kiwi na toothpicks.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa kuwa Mkoa wa Njombe unazalisha viazi kwa wingi, naiomba Serikali itafute wawekezaji kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha kutengeneza bidhaa zinazotokana na viazi kama crisps, katika Mkoa wa Njombe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wafanyabiashara wananyanyasika sana na TRA kutokana na kuwa na tozo nyingi, naiomba Serikali iangalie namna ya kuwasaidia wafanyabiashara wasikatishwe tamaa kwa kukimbizwa na tozo nyingi na hasa kwa wafanyabiashara wadogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wadogo wadogo (wajasiliamali) wa Njombe watafutiwe eneo rafiki kwa ajili ya kufanyia biashara zao. Napendekeza eneo hilo liandaliwe maeneo ya stendi mpya iliyopo Mji Mwema.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.