Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu na kiti chako, napenda kuchangia Wizara hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara hii inahusisha pia uwekezaji ambao kwa kiasi kikubwa uwekezaji bado haujapewa kipaumbele. Kwa kiasi kikubwa hotuba ya Waziri Mheshimiwa Mwijage imejikita katika kuzungumzia viwanda ambavyo kwa kiasi kikubwa ni mbwembwe kuliko uhalisia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Taasisi zote za Umma zenye mitaji ya umma ilitakiwa tuelezwe, kwa kuwa taasisi hizi, mfano Mifuko ya Hifadhi yote inajikita katika uwekezaji. Kwa kiasi kikubwa uwekezaji huu hauna tija. Nilitegemea hotuba ya Mheshimiwa Waziri ieleze juu ya uwekezaji butu unaofanywa na Mifuko ya Hifadhi za Jamii pamoja na Taasisi za Serikali kama vile Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, ununuzi wa viwanja bei ni za juu, hifadhi za Jamii kama LAPF wamenunua Kiwanja Mwanza Square metre moja kwa Sh.255,000/= kitu ambacho siyo kweli. Kuna harufu ya matumizi mabaya ya Ofisi. Mtwara wamenunua kiwanja eneo la Rahaleo Square metre moja ni Sh.155,000/= eneo ambalo mimi nalijua. Niliwaambia haya, wakasema valuer ameruhusu. Valuers wanacheza deal na wahusika. Tunataka uwekezaji wenye tija kama Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimeingia mkataba wa miaka 50 na mwekezaji kutoka Botswana. Huu mkataba unampa mamlaka ya kukusanya kila anachokipata na kuipa Serikali asilimia 10% tu. Hali hii haikubaliki. Kibaya zaidi, anajenga vibanda na anakusanya billions of money. Hivi baada ya miaka 50 vibanda vile vitakuwa na thamani kweli?

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri apitie uwekezaji unaofanywa na Taasisi za Umma sio kuwaza viwanda vya watu ambao yawezekana wasije kabisa kujenga. Hivi vilivyopo vifanyiwe uhakiki wa kina.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumuuliza Waziri, Mheshimiwa Mwijage, Kiwanda cha Mbolea Mtwara kina tatizo gani? Kwa nini hakijengwi wakati mwekezaji yupo tayari? Kwa nini hawawezeshwi kujenga kiwanda hicho? Kwa nini hawampi rasilimali anazotaka ili ajenge kiwanda Mtwara? Kila kitu kipo mpaka kwenye eneo, kigugumizi cha nini au Mheshimiwa Waziri hataki maendeleo ya Mtwara?

Mheshimiwa Naibu Spika, Mtwara Mjini kulikuwa na Viwanda vingi vya Korosho, vyote sasa hivi havipo. Baya zaidi kilikuwepo kiwanda cha OLAM, mwekezaji aliwekeza Mtwara Mjini na kiwanda hiki kilikuwa kinaajiri wananchi wengi sana, lakini Serikali ilimwekea mazingira mabaya ya kodi; huyu mwekezaji, amehamisha kiwanda na kukipeleka Msumbiji. Kwani kuna nini wawekezaji wa Mtwara hamwataki wawekeze Mtwara? Au Wizara inataka Mheshimiwa Rais aje tena Mtwara atamke aliyotamka tarehe 4 Machi, 2017? Naomba wawekezaji wenye nia ya kuwekeza Mtwara wapewe mazingira rafiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu third party katika ajira, UCC Dangote Mtwara; kuna usumbufu mkubwa kiwanda cha Dangote kwa kuwa kuna mtu kati anaitwa UCC ndio anayesimamia na kuajiri watu, baadaye anampa mahindi na mahindi anampeleka Dangote. Hawa watu wakati wanapokonya haki za waajiriwa kiwandani, wananyanyasika sana, wafanyakazi hawana utaratibu, wanadhulumiwa haki zao wakidai mwajiri anasema hawamhusu na anamwambia UCC wafanyakazi kadhaa hawatakiwi na wanafukuzwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza, Serikali ilitoa waraka mwaka 2014 wa kuzuia mtu kati kutoa ajira ya mawakala, umefikia wapi?