Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi sana kwa Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa juhudi zake nzuri za kufufua na kujenga viwanda katika nchi yetu ya Tanzania. Tumeona jitihada kubwa ya Serikali ya Awamu ya Tano. Nakubaliana kabisa kuwa nchi ya Tanzania ni tajiri sana, ina kila kitu, lakini tatizo kubwa ilikuwa ni maamuzi magumu tu. Sasa tumepata Rais mwenye maamuzi magumu na sahihi. Serikali haijengi viwanda, lakini Serikali inasaidia katika kutoa miongozo ya kujenga viwanda na kuvutia wawekezaji kuja kuwekeza Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mufindi Kusini tuna viwanda vingi sana kwa mfano, Kiwanda cha Chai (Uniliver Tea Company Limited), Mufindi Paper Mill Limited (MPM); Mufindi Tea Company Limited. (MTL), Kiwanda cha Pareto, Kiwanda cha Mbao (Sao Hill); pia kuna viwanda vidogo vidogo vingi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri kwa Serikali, naomba Serikali ijenge miundombinu ya barabara, umeme na maji ili kuwezesha wawekezaji kufanikisha uzalishaji wa bidhaa bila matatizo. Viwanda vinashindwa kusafirisha bidhaa kwa sababu ya babaraba mbovu. Barabara hiyo ni Mafinga hadi Mgogolo, Nyololo hadi Mtwango. Kuna tatizo kubwa la stendi ya reli pale Mgololo ili bidhaa ziweze kusafirishwa kwa njia ya treni.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono. Ahsante.