Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia bajeti iliyoletwa Mezani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, nianze kumshukuru sana Mwenyezi Mungu ambaye ameniwezesha kurudi tena kwa mara ya pili katika Bunge hili maana bila yeye nisingekuwemo.
Kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kuchangia bajeti hii, naomba kwanza nishukuru na nikipongeze sana Chama changu cha Mapinduzi kwa ushindi wa kishindo na niwapongeze Wabunge wote wa Chama cha Mapinduzi. Vilevile niendelee kumpongeza Rais wetu, Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa ambayo amekuwa akiifanya. Nimpongeze pia Waziri Mkuu na Mawaziri wote wamekuwa wakifanya kazi nzuri na kwa umakini mkubwa sana. Nimpongeze Spika, nikupongeze na wewe Naibu Spika, nipongeze pia na Wenyeviti wote wa Bunge kwa kazi nzuri mnayoifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze pia Rais wa Zanzibar kwa ushindi wa kishindo kikubwa alichokipata kwenye uchaguzi wao na sasa hivi Baraza la Uwakishilishi ni wana-CCM watupu. Najua sasa watafanya kazi nzuri sana kwa sababu tulipokwenda China labda niwakumbushe wenzangu walioenda China wenzetu wa China walisema kwamba Tanzania mnachelewa kwa sababu ya upinzani. Wenzetu kule chama ndiyo kinachoongoza Serikali, kwa hiyo tulivyokwenda hata na wapinzani walisema kwamba hawa kazi yao ni kuwinda yale mabaya. Kwa hiyo, naamini kwamba Zanzibar watafanya kazi nzuri sana, waendelee kufanya kazi wawakilishe vizuri chama chetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee pia kushukuru tu, naipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa ujenzi wa daraja la Igumbilo ambalo lipo katika Jimbo la Iringa Mjini. Lile daraja kwetu lilikuwa ni tatizo kubwa. Kila mwaka watu walikuwa wanakufa kwenye lile daraja kwa sababu kuna shule ya sekondari, kuna chuo sasa ujenzi wa lile daraja najua kwamba maafa ya vifo vya kila siku pale Iringa tumekombolewa. Kwa hiyo naamini kwamba uchaguzi ujao, najua Mama Mbega alitolewa kwa ajili ya lile daraja, tumeshajenga Jimbo litarudi tu kwenye Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee pia kuchangia kuhusu ucheleweshaji wa fedha za miradi katika Halmashauri zetu. Kumekuwa na ucheleweshwaji mkubwa sana wa fedha za miradi katika Halmashauri na kusababisha miradi hii kuongezeka gharama kwa kiasi kikubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Manispaa yetu ya Iringa Mjini uko mradi ule wa machinjio ya kisasa wa Ngelewala. Ule mradi kwa kweli ulipoanza gharama yake ilikuwa ndogo lakini sasa hivi kadri unavyocheleweshwa ule mradi unaendelea kuongezeka gharama. Kwa sababu mpaka mwaka jana bajeti iliyopita tulitakiwa tutumie shilingi milioni 700 ili kumaliza mradi ule, lakini sasa hivi zinahitajika shilingi 1,400,000,000 ili mradi ule uishe.
Mheshimiwa Naibu Spika, ule mradi utatunufaisha sana sisi Wanairinga kwa sababu kwanza tunategemea kupata ajira kama ya vijana 200 mradi utakapokamilika. Vilevile tunajua kwamba mradi ule utakapokamilika Halmashauri yetu itaongeza mapato. Pia kwa sababu yale ni machinjio ya kisasa tunategemea kwamba nyama itakayochinjwa pale itasafirishwa nje tutaongeza pia pato la fedha za kigeni. Kwa hiyo, labda Serikali ingefanya upembuzi yakinifu kuangalia ile miradi ambayo itasaidia kuongezea mapato kwenye nchi hii au kwenye Halmashauri zetu, hii ingemalizika kwa haraka zaidi ili iweze kutusaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee pia kuchangia kuhusiana na Serikali kutokamilisha miundombinu katika wilaya zetu. Katika Mkoa wetu wa Iringa, Wilaya ya Kilolo, nilishawahi kuuliza swali la nyongeza kwamba ilipata hadhi mwaka 2002 lakini mpaka leo miundombinu yake mingi sana bado haijakamilishwa katika makau makuu. Kwanza, Jimbo lile lina changamoto kwamba kuna wananchi wanaoishi mabondeni na kuna wanaoishi milimani. Kwa hiyo, utakuta kwamba kutokuwepo miundombinu kwenye makao makuu wananchi wanapata shida sana. Hakuna Hospitali ya Wilaya ya Serikali, hakuna Mahakama, Mahakama ya Wilaya wanaendeshea kwenye Mahakama ya Mwanzo. Vilevile Makao Makuu ya Polisi hayapo katika Makao Makuu ya Wilaya. Kwa hiyo, Serikali ingeangalia kwa sababu nia ya Serikali kuanzisha Wilaya ni kusogeza huduma kwa wananchi. Sasa kama hamuweki huduma kwa wananchi hata ile nia ya kuanzisha hizo Wilaya inakuwa bado haisaidii kitu chochote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niwazungumzie wazabuni. Madeni ya wazabuni kwa kweli yamekuwa mwiba sana. Wazabuni wengi wanadai sana na wengi wao kwanza wamekopa benki na wengi wao wanadaiwa mpaka kodi za mapato. Kwa hiyo, sasa nia ya kuwasaidia hawa wananchi wenye kipato cha chini inakuwa hamna kwa sababu kama wamekopa wakauziwa zile dhamana zao kwa ajili ya madeni ambayo wanadai Serikali naona itakuwa hatuwasaidii. Kwa hiyo, naomba suala hili lipewe kipaumbele ili wazabuni kwenye halmashauri zetu zote au kwenye Serikali yetu yote waweze kulipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine labda nielezee kuhusu barabara zetu za Halmashauri. Kumekuwa na tofauti kubwa sana kati ya barabara za Halmashauri na za TANROADS. Huwa najiuliza ni kwa nini kwa sababu hata kule kuna wataalam, labda kama mnapeleka pesa kidogo mngepeleka pesa nyingi ili na zenyewe ziwe na uimara kwa sababu barabara za Halmashauri zinajengwa temporary sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa…….
NAIBU SPIKA: Kengele ya pili hiyo Mheshimiwa.
MHE. RITTA E. KABATI: Naomba niunge mkono hoja.