Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda na elimu. Kulingana na umuhimu wa kuwa na viwanda nchini kwetu, ni lazima kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kuanzisha viwanda na faida zitakazopatikana baada ya kuwa na viwanda nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuboresha kilimo. Kulingana na utaratibu wa viwanda ni vyema wananchi wakabadili utaratibu wa kilimo cha mazao na badala yake walime au kuanzisha kilimo chenye tija kwa ajili ya kuhudumia viwanda vitakavyokuwa vinazunguka maeneo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda na ajira kwa vijana. Ili suala la viwanda lifanikiwe ni vyema elimu ikatolewa zaidi kwa vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa ambao watanufaika na viwanda badala ya kuchukuwa vijana wa nje ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzisha elimu ya viwanda mashuleni. Kulingana na umuhimu wa suala la kuanzisha viwanda ni vyema kama wanafunzi katika masomo wakawa na elimu au mada juu ya kuanzisha na kuendeleza viwanda nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuwawezesha wakulima. Kwa kuwa viwanda vingi na kwa asilimia kubwa vinategemea kilimo na ili suala hili la viwanda lifanikiwe ni vema wanawake wakulima wawezeshwe kuanzisha viwanda hata kama ni vidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda na mazao ya biashara. Ni vema Wizara ya Viwanda na Biashara kuwa na mkakati wa kudumu na endelevu kwa kuwa na viwanda bora vya kuandaa mazao ya biashara ili kilimo kiweze kuwakomboa wakulima wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzisha vyuo vya VETA Mkoa wa Rukwa. Vyuo hivi vitasaidia vijana kupata ujuzi utakaosaidia kuendesha viwanda vitakavyoanzishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, masoko ni tatizo kubwa kwa wakulima hasa wa Mkoa wa Rukwa mpaka wanaelekea kukata tamaa kutokana na changamoto hii. Naomba Serikali ishughulikie suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Serikali ifufue viwanda vilivyokufa vya nguo, nyama, maji na kilimo (pembejeo).

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.