Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS:Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Allah Subhanahu Wataala kwa neema ya uhai na afya njema. Nikushukuru wewe pia kwa nafasi hii muhimu sana kwangu ili nitoe mchango wangu ingawa kwa ufupi katika Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze na bidhaa bandia. Pamoja na kwamba Serikali kupitia (TBS) imeweka program ya kudhibiti bidhaa bandia kutoka nje ya nchi lakini kinyume chake bidhaa bandia zinazagaa kila sehemu ya nchi yetu, wakati mamlaka ya udhibiti (TBS) wapo na jambo hili wanalijua na hakuna hatua madhubuti zinazochukuliwa. Jambo hili la bidhaa bandia linaweza kuleta madhara makubwa katika nchi na kwa wananchi wenyewe kwa ujumla. Pamoja na kuzorotesha bidhaa za ndani ya nchi lakini pia wananchi hawana elimu ya kutosha juu ya jambo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu juu ya jambo hili ni kwamba, kwa sababu (TBS) wanashughulikia bidhaa bandia, na kwa kuwa (TBS) hawana uwezo wa kushughulikia bidhaa bandia na kwa kuwa (TBS) hawana uwezo wa kushughulikia na bidhaa fake na kwa sababu (TFDA) pamoja na mambo mengine inajishughulisha na dawa zilizokuwa chini ya kiwango na kwa sababu (FCC) inashughulika na bidhaa fake, kwa mantiki hiyo ni bora taasisi hizi kufanya kazi kwa pamoja ili kuleta ufanisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la ngozi. Tanzania tuna ng’ombe million 21.3; mbuzi millioni 1.5; na tunao kondoo millioni 6.4. Pamoja na kuwa na mifugo mingi kiasi hiki jambo la ajabu Tanzania tunasafirisha ngozi ghafi katika kiwango ambacho hakiendani na rasilimali tuliyonayo ukilinganisha na Kenya ambayo inasafirisha ngozi ghafi nyingi kuliko Tanzania. Pia Sekta ya ngozi haitengenezi ajira wala haiongezi pato la Taifa kwa hiyo inachangia pato kidogo sana la Taifa. Pamoja na juhudi za Serikali za mara kwa mara za kuongeza kodi mpaka kufikia asilimia 90 ili kuzuia usafirishaji wa ngozi ghafi nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, mpango huu haujasaidia kwa sababu bado ngozi zinasafirishwa kwa magendo hivyo kukosesha mapato ya Serikali kutokana na kodi iliyowekwa. Pia hata ngozi ingebaki ndani ya nchi zingeoza kwa sababu hakuna viwanda vya ku-process ngozi wenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali iweke mkakati wa makusudi wa kuokoa sekta hii ya ngozi. Kama si hivyo basi wingi wa mifugo tulionao hautasaidia vema uchumi wa nchi yetu. Tutabaki na changamoto zile zile za siku zote kati ya wakulima na wafugaji kugombania malisho. Naomba tuwe makini kuhusu hili.