Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia Wizara hii muhimu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Nimefuatilia sana taarifa ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji lakini katika hotuba yake hakuzungumza mkakati wa kufufua viwanda vilivyokufa.

Mheshimiwa Naibu Spika, wazo la Tanzania ya Viwanda lilikuwepo na Mwalimu Nyerere miaka 1967 alikuwa na vision hiyo na ali-implement wakati ule kwa kuhakikisha viwanda vingi vinaanzishwa katika mikoa mbalimbali ukiwemo mkoa wa Morogoro. Mkoa wa Morogoro pekee ulikuwa na viwanda zaidi ya 40, lakini hivi sasa viwanda vingi vimekufa vikiwemo viwanda vya Canvas, Komoa, Asante Moprocco, Ceramic Tanzania, Leather Shoe, Unnats na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa aje na majibu, upi mkakati wa Serikali wa kufufua viwanda vya Mkoa wa Morogoro ambavyo vilikuwa vikitoa ajira kwa wananchi wa Mkoa wa Morogoro?

Mheshimiwa Naibu Spika, ubinafsishaji wa viwanda ulikuwa na lengo la kuongeza ufanisi wa uzalishaji na si kuua viwanda. Sasa kwa nini uwekezaji umetumika kuongeza tija kwa mwekezaji na kuua ajira? Wawekezaji kwa masikitiko makubwa wametumia viwanda hivi kama Collateral kuchukua mikopo mikubwa katika mabenki badala ya kuendeleza kwenye biashara za malori, mabasi na kuua viwanda hii sio sawa. Tunataka kuona Serikali inachukua hatua mahsusi kwa wawekezaji hao kwa makusudi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nyumba za Serikali zilizonunuliwa na wawekezaji hata baada ya kuua viwanda kwa nini wawekezaji hawa wasirudishe nyumba hizo zikatumika kwa wafanyakazi wa Serikali? Hawalipi kodi hawalipi pango, huku wameua viwanda; ni kwa nini Serikali isichukue nyumba hizi zikatumika kwa maofisa wa Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, biashara ya Mwendo Kasi Jiji la Dar es Salaam, ni kama imekuwa monopolized na watu wachache. Kabla ya mwendo kasi wapo wamiliki wa mabasi ya daladala ambao walikuwa wakifanya biashara tena kwa mkopo na wengine wakijifunga mkanda kuuza nyumba, mali na kuingia kwenye biashara ya daladala. Serikali imekuja na mpango wa mabasi yaendayo kasi; kwa nini wasiwape fursa wafanyabiashara wa daladala nao kama wana uwezo wawekeze katika mabasi hayo?

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa mabasi ya mwendo kasi ambayo yalikuwa yanatoa huduma kwenye njia pekee sasa hivi yanafanya biashara kwenye njia ambazo si maalum; wa mfano Mbezi Louis, Muhimbili; hali hii inawaweka pembezoni wafanyabiashara wanyonge wa daladala ambao nao wangeweza kupata fursa hizo kama wazawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tafsiri ya viwanda sasa itekelezwe kwa vitendo ambapo tunatarajia kuona Serikali inafanya kazi kwa pamoja na Wizara nyingine mtambuka kama vile Wizara ya Kilimo na Mifugo, Nishati na Madini pamoja naWizara ya Maji na Umwagiliaji. Hakuna viwanda bila uhakika wa umeme na malighafi.