Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze mapema kabisa kuanza kuiunga mkono hoja iliyopo mezani ili nisije nikasahau. Vilevile nitumie nafasi hii kutoa pongezi sana kwa Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yake kwa hotuba nzuri, lakini vile vile kwa jitihada kubwa ambayo ameonesha katika kutupeleka katika nchi ya viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, yeyote yule anayebeza jitihada za Mheshimiwa Waziri na Timu yake, najua atafanya hadharani lakini nina hakika kimoyo moyo anampongeza. Kwa sababu haiwezekani kwamba ndani ya kipindi cha mwaka mmoja na nusu tu tayari tunashuhudia uanzishwaji wa viwanda zaidi ya 300. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wakati wanachangia, wameibua masuala yanayogusa kilimo ambayo ningependa kuyatolea ufafanuzi kwa muda mfupi nilionao. Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wameongelea kuhusiana na biashara ya chakula na bidhaa zinazotokana na kilimo katika ukanda wetu wa Afrika Mashariki, wakiashiria kwamba wangetaka na sisi tufuate kinachofanyika kwenye nchi nyingine kuagiza chakula kutoka nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwafahamisha Waheshimiwa Wabunge kwamba pamoja na changamoto ya chakula tuliyopata katika mwaka uliopita, lakini ukifananisha na picha tuliyonayo katika ukanda wetu wa Afrika Mashiriki, nchi yetu imeendelea kuwa na hali nzuri ya chakula kuliko nchi yoyote katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukichukua baadhi tu ya bidhaa za chakula tutaona picha kuhusiana na hali halisi ya bei kwa sasa. Tukichukua zao la mahindi, bei ya wastani Uganda tunavyozungumza leo ni Sh. 96,000/=, wakati Kenya ni Sh.114,000/=; Rwanda ni Sh.88,000/=, Juba au Sudani ya Kusini ni Sh.135,000/=, Burundi ni Sh.152,000/= wakati kwetu bei ya wastani kwa leo ni Sh.95,000/=. Kwa hiyo, unaweza ukaona tumekaaje katika mizania ya kikanda ikija suala la bei ya mahindi. Hata zile nchi nyingine ambazo zinaelekea zina bei nzuri kama Rwanda ni kwa sababu wao wameagiza kutoka Brazil. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile tukiangalia zao la mchele au basi chakula cha mchele, tunaona kwamba bei ya wastani Uganda kwa leo ni Sh.203,000/=, Kenya ni Sh.267,000/=, Rwanda ni Sh. 204,000/= lakini Burundi ni Sh.236,000/= na kwetu bei ya wastani wa mchele kwa leo ni Sh.174,000/=. Unaweza ukaona kwamba bado sisi tukiangalia kikanda tuko katika hali nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile imezungumzwa sana kuhusu sukari. Ukiangalia bei ya sukari katika Nchi za Afrika Mashariki, utagundua kwamba nchi yetu bado tuko katika hali nzuri ukifananisha na nchi za jirani. Bei ya wastani Burundi kwa leo ni kati ya Sh.3,700/= mpaka Sh.4,000/=; Uganda kati ya Sh.3,500 mpaka Sh.4,000/=; Kenya ni kati ya Sh.3,500/= mpaka Sh.5,000/=. Kwa hiyo, ukiangalia sisi Tanzania tuko katika hali nzuri bei ya sukari ni kati ya Sh.2,500/
= mpaka Sh.3,000/=.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo asubuhi nilipata wasaa wa kuongea na Ma-DC wa Wilaya za mpakani za Kakongo, Misenyi, Ngorongoro, Rombo na Tarime, kujaribu kuangalia hali ya chakula na kimsingi wote wanasema kwamba sisi kama nchi bado tuna hali nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge waliokuwa wanataka na sisi tuagize chakula kutoka nje, wangeshauriwa vizuri zaidi kuhusiana na athari ambazo nchi yetu ingeweza kupata kwa kufanya kama hivyo. Kimsingi Kenya na Rwanda wao wameagiza chakula kutoka nje kwa sababu wao wana changamoto kubwa ya chakula, hali yao ya chakula siyo nzuri; wakati sisi mwaka uliopita tulikuwa na ziada ya tani milioni tatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tathmini ambayo tumeifanya karibu mikoa yote inatuonesha kwamba mwaka huu inaelekea kwamba tutapata chakula kingi zaidi. Sisi hatuna haja ya kuagiza. Kenya wameagiza chakula kutoka Mexico kwa sababu hali yao ni mbaya, lakini kawaida wao wanategemea Tanzania na Uganda katika kupata chakula.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.