Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Rashid Ali Abdallah

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tumbe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha leo hii kusimama hapa. Mchango wangu wa leo si mkubwa nitazungumza mada fupi kwa sababu tayari nilishachangia kwa maandishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo langu kubwa ambalo naliona katika kilimo ni wakulima wadogo wadogo, Wabunge wote wanawaona wanavyohangaika katika kilimo; mvua, jua, usiku na mchana na mazao yao tunayaona barabarani yanavyooza. Huu ni mtindo wa kila mwaka. Wakulima wanalima wanatumia nguvu zao jasho lao ni maskini kabisa, lakini hatimaye mazao yao yanapotea ovyo. Serikali wanaona, Mheshimiwa Magufuli Rais, alikuwa ni Mbunge alikuwa anapita barabarani anaona mazao yanavyooza lakini amechukua hatua gani? Soko liko wapi la wakulima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri kama anataka kutumikia Taifa hili kwa kilimo tafadhali awajali wakulima wadogo wadogo. Wakulima wadogo wadogo ndio wanaoleta maendeleo ya Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije katika Uvuvi wa Bahari Kuu. Uvuvi wa Bahari Kuu kwa taarifa za Waziri kwamba wanatoa leseni kwa dola elfu 50 kwa mwaka. Meli zinakwenda kuvua huko kwa samaki wanaotaka wenyewe na wale wa ziada wanawapoteza, kuna meli za uvuvi mia moja na tano kwa taarifa ya Waziri. Wanavua bahari kuu wanachukua samaki wanaowataka wa ziada wanawapoteza. Serikali ina utaratibu upi wa kuweza kulinda mazao haya ambayo yanaingiza fedha za kigeni kwa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara imetulia kimya Waziri mwenyewe anasema, anawaagiza, samaki wa ziada mlete juu kama vile ni kampuni yake. Kuna sheria ipi ya kuhakikisha samaki wale wa ziada wanaletwa huku katika nchi yenyewe. Kwa hiyo, wanakwenda katika vyombo vya habari anazungumza na Waandishi wa Habari, anawaambia samaki wa ziada leteni nchini huku. Hasa watu watoe meli zao huko deep sea walete huku nchini wapoteze mafuta yao bure, kuna utaratibu upi ulioweka Mheshimiwa Waziri kuweza ku–save mapato haya ya Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, kuna masuala haya ya migogoro ya wakulima, migogoro hii inazidi kukua kwa Wakulima na Wafugaji. Tuna hekta milioni 88. Kati ya hekta milioni 88 kuna hekta milioni 60 ambazo zinafaa kwa wafugaji. Hata hivyo, unit tulizonazo za ufugaji ni unit bilioni 20 lakini mahitaji yetu ni unit 17.1 tuna tatizo gani la kuweza kuondoa mzozo huu wa wakulima na wafugaji. Kwa hiyo Serikali imetulia kimya tu. Mmechukua hatua gani watu wanauwana, mifugo inakufa, mizozo yao hii haishi. Uwezo wa kuweza kuyatatua tunao, kitakwimu tunafanya kazi.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ana dhima kubwa ya kuhakikisha kwamba mizozo hiyo ya wakulima na wafugaji wakishirikiana na Wizara nyingine inatatuliwa ili ku– ave maisha ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, masuala ya mbolea, Serikali hii imekuja na dhana ile ya viwanda na kila ninavyoona ninavyopima tafsiri ya kilimo kwanza imeondoka. Kwa hiyo dhana iliyopo ni ya viwanda, sasa matokeo yake ni nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015/2016, Awamu iliyopita ilitoa mbole na pembejeoyenye dhamani ya bilioni 78, lakini mwaka 2016/2017, Awamu ya Mheshimiwa Rais Magufuli wametoa bilioni 10 hii inaonekana kama ni dharau hivi! Bilioni 78 ambapo wakulima wenyewe wamelalamika kwamba hazikutosha, leo Serikali hii imeweka bilioni 10, is nothing. Hii ni dharau kwa wakulima, kama hukutia mbolea basi mazao yatapungua. Mvua tumepata za kutosha lakini mvua pekee hazitoshi, lazima tuzi-support na mbolea na nina imani kwamba mazao kipindi yatapungua kwa sababu mbolea kipindi kilichopita haikutosha, wala haikufika kwa wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi ya chakula; wakulima wamelima kipindi kilichopita na kwa bahati nzuri wakapata mazao mengi, wakazuiliwa kabisa kusafirisha mazao yao nje. NFRA wakanunua mazao tani milioni 13 something ambazo zina thamani ya bilioni sita. Zimekuwa declared kwamba zimeharibika kwa mvua kwenye maghala. Waziri mwenyewe anasema katika maelezo yake kwamba zile tani hazikuharibika, ni watu wamefanya michakato yao tu. Waziri anajua, amechukua hatua gani kwa watu hawa?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha ya Serikali imepotea bilioni sita (6) na zaidi, mazao ya wakulima yamenunuliwa na yalizuiliwa kupelekwa nje, wakulima wamepewa fursa zote halafu wahuni wanasema yamenyeshewa na mvua lakini hadi sasa hakuna hatua iliyochukuliwa. Mheshimiwa Waziri nataka kujua fedha ya umma iliyoharibika kwa uzembe wa stoo hizi za NFRA na kupoteza bilioni sita, watu hawa wamechukuliwa hatua gani?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba, kama tutakwenda hivi katika kila Wizara kama haipo serious na nguvu za wakulima haipo serious na kuwasaidia wakulima, haioni huruma, nataka Waziri hebu tumpe hekta moja tu au robo heka tu aende akalime, amwagilie maji avune mazao yake, halafu mazao yale yaharibike arudi tena mwaka wa pili alime tena na hakuna support yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la wafugaji, mara hii tumeona kwamba ng’ombe wengi wamekufa, lakini Mheshimiwa Rais Magufuli anawaambia nendeni mkauze ng’ombe akauze wapi ng’ombe? kwani ng’ombe wanauzwa vipi. Ng’ombe wanakufa kila maeneo hakuna malisho, lakini sasa hizi mvua zinavyonyesha utakuta majani yamezagaa tele, hakuna utaratibu wa ku-process majani yale. Kuna mashine nyingi unavuna majani unaweka katika stoo wakati wa kiangazi Serikali inapata mapato wanauzia wakulima ambao hawana majani, majani mashambani yanapotea bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mashine ya kuyasindika majani yale ziko tele na ni rahisi. Serikali imekaa tu, fedha ile pale na ng’ombe wanakufa, mifugo inakufa, watu wametulia hapa, wanakwenda huko na kurudi, tujenge raslimali yetu kwanza, tutunze rasilimali yetu, tutunze kilimo, tutunze mifugo, zile initiative tulizonazo tuzitumie hizo kwanza usianzishe viwanda vikubwa lakini viwanda vidogo vya wakulima huku wanakufa, wewe unaanzisha viwanda vikubwa tu, what for ? Maana yake nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajira ya kilimo ni asilimia 65.5 kwa mujibu wa taarifa zako, wengine wanasema asilimia 75 sijui who is wrong kama Waziri yuko sahihi au tuzungumze hapa, lakini vyovyote itakavyokuwa ni kwamba sekta ya kilimo inabeba Taifa. Kwa sababu inabeba Taifa Sekta hii ya kilimo nguvu za Awamu hii ya Tano ziko wapi, hatujaziona, tunasikia zimeagizwa matrekta lakini, hebu kwanza tuimarishe kilimo. Kilimo ndiyo uti wa mgongo wanasema, kilimo ndiyo maisha.