Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza natoa shukrani zangu za dhati kwa Rais wa Awamu ya Tano Mheshimiwa John Magufuli kwa imani na uwezo mkubwa alionao katika kuendeleza Taifa letu. Pia napenda kuwapongeza Mawaziri wote kwa juhudi wanazoonesha katika kuendesha Wizara zao. Vile vile nachukua nafasi hii kuwashukuru wananchi wote wa Jimbo la Tumbatu kwa imani waliyonipa kwa kunichagua kuwawakilisha katika Bunge lako Tukufu. Naahidi nitaendelea kuwatumikia kwa uwezo wangu wote.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, napenda kutoa mchango wangu katika sehemu ifuatayo:
Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma; Katika sehemu hii imeelezwa kuwa, Serikali imetoa elimu kwa Viongozi wa Umma wapatao 3,980 katika sehemu tofauti, ikiwemo Walimu kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, mgongano wa maslahi na maadili ya Utumishi wa Umma kupitia semina, midahalo, mafunzo na vikao mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu katika sehemu hii naiomba Serikali ieleze ni Viongozi wa ngazi gani walipata mafunzo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante.