Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata fursa hii adhimu ya kuweza kuchangia Wizara hii muhimu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii inachukua asilimia 80 ya Watanzania yaani ukiangalia wakulima, wafugaji na wavuvi ni almost asilimia 80, asilimia 20 ndiyo ya Watanzania wanaofanya shughuli nyingine. Sekta hii isipoangaliwa kwa umakini wa hali ya juu ni dhahiri kabisa kwamba tunaweza tukaliingiza Taifa kwenye mgongano wa wenyewe kwa wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasikitika sana, nchi hii imejaliwa maeneo mazuri, ardhi nzuri, mito, bahari, mabonde, milima na kila kitu na asilimia kubwa ya ardhi bado iko vijijini na wakulima na wafugaji wengi bado wapo vijijini, ni tatizo gani linalotushinda kama nchi kuweka sera nzuri zitakazohakikisha kwamba Taifa haliingii kwenye migogoro? Tuna Land Use Planning, tumejipanga kila kitu, kwa nini watu wanagombana, shida iko wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kuna sababu za kijiografia zinazopelekea watu wanahama na mifugo kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Kuna maeneo ambayo kwa mvua jinsi ilivyonyesha mwaka huu mifugo haiwezi ku-survive mafuriko lazima watahama kutoka eneo moja kwenda eneo lingine. Tumeona nchi nzima mvua inanyesha lakini Dodoma hii kuna maeneo kabisa mvua haikufika automatically lazima wakazi wa maeneo hayo ama wafugaji wa maeneo hayo ku-shift kutoka hapa kwenda sehemu nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni wakati gani mfugaji huyu atakwenda kuomba kibali cha kuhakikisha kwamba anahama na mifugo yake na wakati mifugo wale wanatakiwa ile ili wasife na njaa? Kwa hiyo, tunapoweka sera, sheria na sheria ndogo lakini lazima tuhakikishe mabadiliko ya kijiografia ambayo yanaweza yakapelekea watu wetu waweze kuhama yanazingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nizungumzie suala la uvuvi. Mkoa wa Kigoma tuna Ziwa Tanganyika na lina samaki wa aina nyingi sana lakini samaki wale kwa kweli hawavuliwi ipasavyo. Tuna dagaa wazuri ambao wanapelekwa Uingereza, Marekani, Malaysia na sehemu zingine lakini bado wanavunwa kwa kiasi kidogo sana. Tunaomba kujua Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia vijana wetu na wavuvi wanaotoka Ziwa Tanganyika waweze kuvua uvuvi wenye tija na kulisha nchi lakini pia na kulisha nchi za nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna shida kwa wavuvi wetu katika Ziwa Tanganyika wanatekwa na maharamia kutoka Congo na wengine kutoka Burundi wakiingia kule wananyang’anywa nyavu zao, pesa, mashine na kadhalika. Hali hii inawarudisha vijana wengi nyuma na kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi kwa kuhofia usalama wao. Serikali inawa-guarantee vipi vijana hawa ambao wana-risk kwenda kutafuta maisha katika ziwa lenye kina kirefu kuhakikisha kwamba wanafanya kazi kwa ufanisi mkubwa na kuweza kuchangia uchumi wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia bado kodi kwa wavuvi ni kubwa. Nilikuwa na-discuss na Mheshimiwa hapa wa Ukerewe, wavuvi wanatozwa kodi kubwa sana za uvuvi, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza kodi hizi? Kwa sababu mvuvi anapokwenda kuvua kwanza kuna mawili, aidha, arudi salama ama asirudi salama. Kwa hiyo, pamoja na kuchukua risk yote hii kwa nini tunawatoza tozo kubwa na ni za kero? Mna mkakati gani wa kuhakikisha kwamba tunapunguza kodi za kero kwa wavuvi wetu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mkoa wa Kigoma tunalima, tuna zao la mchikichi. Kwa taarifa ya research zilizofanyika hivi karibuni, zao la mchikichi linatumika katika kuzalisha bidhaa mbalimbali katika nchi ya Europe kwa asilimia 80. Chocolate hizi zinazotengenezwa ili ziweze kuganda na ziweze ku-survive zinatumia zao la mchikichi, lakini hakuna utaratibu wowote unaowekwa kuhakikisha kwamba unafanyika utafiti wa kutosha na zao hili liweze kulimwa kwa umakini wa hali ya juu.