Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. OMAR A. KIGODA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kumpongeza Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa utendaji wake, pia kulitakia kila la kheri Baraza la Mawaziri katika kutekeleza Ilani ya Chama Tawala.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na hotuba ya Mheshimiwa Waziri, napenda kujikita kwenye ushauri. Kwanza; Serikali ijitahidi kufuatilia kwa karibu fedha ambazo zinakwenda kwenye Halmashauri, bajeti nyingi sana zinapangwa vizuri, lakini inapokuja suala la matumizi huwa zinapotelea Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili; kuwe na uwazi wa mapato ya ndani yanayokusanywa na Halmashauri. Hii itasaidia hata kwa Wabunge kujua ni kiasi gani kinapatikana na kiasi gani kinatumika kurudi kwenye huduma za jamii. Kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi juu ya huduma mbovu kwa jamii kama barabara za mitaa, vyoo na mahitaji mengine madogo madogo ambayo Halmashauri ina uwezo wa kuhudumia.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatu; suala la uajiri wa wafanyakazi ningeshauri pia kuwe na upendeleo wa baadhi ya wafanyakazi wawe wazawa ili kuwe na uchungu wa utendaji. Inaonekana watumishi wengi wa Halmashauri ni watu wanaokuja na kuondoka. Hili pia linasababisha kuzorota kwa maendeleo kutokana na ugeni wao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nne; napenda pia kumshauri Waziri mara kwa mara wawe wanapeleka wataalam kwenye Halmashauri zetu ili kufanya auditing kuangalia matumizi ya hela ambazo ni hela ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.