Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia bajeti hii iliyopo mbele yetu ambayo kimsingi wote tunakubaliana kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa Taifa letu. Nataka nihoji kwa sababu katika mijadala mingi tumekuwa na hoja inayozungumzwa kwamba Serikali ina dhamira njema ya kuwasaidia Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuhoji kwamba dhamira ya kweli ya Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi katika suala la kilimo na mifugo ipo wapi katika bajeti hii? Hivi dhamira ya kweli ya Serikali ni ya kutoa asimilia tatu ya bajeti yake kwa ajili ya sekta ambayo ni Uti wa Mgongo wa Watanzania? Tunataka Serikali ituambie kama asilimia 80 au 70 ya Watanzania ni wakulima na wafugaji, dhamira ya Serikali katika kuwasaidia wakulima na wafugaji hawa iko wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshangaa katika kitabu cha Mheshimiwa Waziri huku wameweka ng’ombe huku mbele na samaki, huku nyuma wameweka kilimo ambacho kinaonesha mazao ya wananchi. Wao wamechangia nini, kwa nini wanajisifu kwa kitu ambacho hawachangii chochote katika kuwanufaisha Watanzania? Nini mmechangia katika mifugo wanaiweka huku wanaona imenawiri sana, nini wanachangia katika kilimo hiki wanachoona mazao yamenawiri sana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka Wizara ituambie hizi picha walizotumia kwenye kitabu hiki copy right yake iko wapi wakati hawachangii chochote, wanatenga bilioni 100 lakini mnapeleka bilioni tatu. Dhamira yao haiwasuti, wanachukua picha ya ng’ombe zetu wanaweka kwenye kitabu chao lakini Wizara hii hawachangii chochote katika kusaidia maisha ya wananchi, hatukubaliani nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili tunataka dhamira ya Serikali katika hili ionekane katika matendo ya kweli, kama dhamira haionekani katika matendo dhamira hiyo imekufa. Katika hili dhamira imekufa kwa sababu hakuna chochote ambacho Wizara imefanya, nchi hii inaongoza kwa mito na maziwa lakini hakuna hata mradi mmoja wa mfano Wizara imeanzisha kwa ajili ya kuonyesha kilimo cha mfano kwa Watanzania. Sasa wanajisifu nini kama Wizara?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Wizara hii inaendelea kukubaliana na utekaji na uuzaji wa mifugo ya wafugaji ambao peke yake katika Wizara hii ndiyo mifugo inauzwa hata bila ya hukumu ya mahakama. Ni mahali ambapo Wizara ya Maliasili inanyanyuka inauza ng’ombe inavyotaka. Ni wapi umeona kwenye nchi hii mali za watu zinataifishwa bila mahakama kutoa hukumu, Wizara imenyamaza. Wizara hii haioneshi ni namna gani inawasaidia wafugaji kuondokana na matatizo yanayowakabili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbaya zaidi mnasema ni uti wa mgongo lakini wameitenga Wizara ya Maji na Mifugo katika bajeti hii hapa. Nataka nishauri Serikali, suala la maji kwa maana ya umwagiliaji lihamishwe kutoka Wizara ya Maji lipelekwe kwenye Wizara ya Kilimo na Mifugo kwa sababu huwezi kuendesha kilimo wala mifugo bila kuwa na maji ya uhakika. Tusipofanya hivyo, tutaona bajeti ya Wizara ya Maji inakuwa kubwa lakini Wizara hii ya Mifugo na Kilimo haitakuwa na chochote na wao hawatatekeleza miradi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inapata kigugumizi gani kuhamisha suala la umwagiliaji ikapeleka kwenye Wizara inayohusika na kilimo ili angalau tuwe na miradi michache kwenye Ziwa Tanganyika, Ziwa Viktoria ili angalau tuwe na miradi michache tunayosema kama nchi tumeweza kuzalisha. Ni nchi pekee tuna maziwa makubwa lakini kiangazi cha miezi miwili tu, mitatu nchi tunalia njaa halafu tunasema kwamba tufanye kazi, kazi ipi ambayo tunafanya kama Serikali haisaidii wananchi wake kuondokana na matatizo tuliyonayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka niishauri Serikali, kumekuwa na tatizo la muda mrefu kati ya wafugaji na wanyamapori lakini wameanzisha na zoezi la kuweka ng’ombe chapa. Ili waweze kufanikisha zoezi hili ni muhimu kuweka miundombinu ya maji katika maeneo ya wafugaji. Kama hawajaweka miundombinu mifugo itahama tu na kama itahama wataishia kutunyanyasa na kutunyang’anya mifugo yetu yote. Nataka niwaambie hawatakuwa wamewasaidia wafugaji ambao wameonekana kama kundi ambalo halina haki katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namba hili suala la kuweka ng’ombe chapa lisimame mpaka Serikali itakaposema ni kwa namna gani imeboresha mazingira katika maeneo haya ambayo wanataka mifugo iwepo. Huwezi kuniambia nichunge ng’ombe mahali ambapo hakuna maji. Bahati nzuri Naibu Waziri naye ni mfugaji, hivi anavyosema aweke chapa ng’ombe kule Ngorongoro wakati hajaweka masuala ya maji katika eneo hilo anategemea wale wapiga kura wake waende wapi? Nataka yeye mwenyewe awe mfano kwa kuisaidia Serikali kuona kwamba hawezi kutenga eneo la mifugo bila kuboresha mazingira ya upatikanaji wa huduma za maji na majosho katika maeneo husika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo langu la mwisho, kwa nini sekta ya mifugo haina ruzuku.