Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kupata nafasi hii nami nichangie Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Jambo la kwanza naunga mkono hotuba ya Kambi ya Upinzani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ni sekta kubwa ya ajira hapa nchini kwetu maana inaajiri takribani asilimia 70 ya Watanzania. Wizara hii hii ndiyo yenye kauli mbiu nyingi tulianza na kauli mbiu ya Baba wa Taifa ya Siasa ni Kilimo, ikaja Kilimo cha Kufa na Kupona cha Mheshimiwa Alhaji Ali Hassan Mwinyi, ikaja Kilimo Kwanza cha Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema siasa ni kilimo maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba kilimo kinagusa maisha ya kila mwananchi, kilimo kinagusa maisha ya kila Mtanzania lakini kilimo hiki hakijamkomboa Mtanzania huyu. Kwa mfano, katika Mkoa wa Mara, enzi za zamani nilipokuwa naenda kijijini kwetu Kabulabula wazee walikuwa wanalima sana pamba na ilikuwa inastawi kwa asilimia kubwa sana na ndiyo maana Mkoa wa Mara ulikuwa una viwanda vingi sana na mazao mengine kama mihogo na viazi vilikuwa vinashamiri sana, lakini sasa hivi wakulima hawa wanahangaika kutokana na uhaba wa mazao haya hayapati rutuba na hayakui.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waziri atakapokuja kuhitimisha atueleze hizi mbegu wanazozileta sasa hivi ni mbegu za aina gani, maana hazikui na zao la pamba limekufa katika Mkoa wa Mara halistawi tena. Mazao ya mihogo zao hili limekufa ni tofauti kabisa maana unapopanda mihogo inapokaa kidogo tu inapata ugonjwa wa ukungu, sasa sielewi hii mihogo inapopata ukungu tatizo ni kitu gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Mara ni Mkoa ambao ulikuwa unategemea kwa kiasi kikubwa kilimo lakini kilimo hiki kinasuasua. Naomba Waziri atakapokuja atueleze ni mbadala wa mbegu zitakazoletwa katika Mkoa wa Mara ili watakapokuwa wanalima kama ni mazao ya pamba, mihogo na viazi vistawi kama vilivyokuwa vinaota zamani. Kwa sababu sasa hivi mkulima akipanda mbegu ya pamba kama ni heka tano, matokeo ya lile zao uvunaji wake ni kama heka moja tu. Tunaona ni namna gani zao la pamba linavyodidimia kutokana na uhaba au ubovu wa mbegu ambazo si stahili.