Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MAGANLAL M. BHAGWANJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi hii kuchangia leo. Kwanza, naomba kuipongeza Serikali kwa kupitia kwa Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na Baraza la Mawaziri, kwa kufanya kazi nzuri na kurudisha imani kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishauri Serikali iangalie zaidi kuboresha Utawala Bora, pamoja na jitihada hizo zilizofanywa ni vizuri kuwe na suala la huduma kwa mteja. Itolewe elimu katika ngazi zote, Tume au Sekretarieti ya Utumishi wa Umma iboreshwe ili waweze kufanya kazi ngazi zote Taifa, Mkoa na Wilaya ila zile kazi za kada ya chini zipewe Halmashauri jukumu la kuajiri.
Mheshimiwa Naibu Spika, muhimu pia tuwe na Maafisa Mipango zaidi katika ngazi zote, Halmashauri, Kata na Vijiji ili miradi iweze kuibuliwa, pia wakiwemo, katika miradi ya TASAF wananchi wapate fursa ya kuibua miradi yenye manufaa kwao. Pia TAKUKURU isaidie kuondoa kabisa rushwa, kero ndogondogo mfano wa traffic barabarani, vibali vya dhamana, kupata leseni, ni mifano michache. Vile vile kwenye elimu, Serikali iangalie namna ya kuboresha na kukomesha shule na vyuo feki ambavyo havitoi elimu kwa viwango na zisizofuata Kanuni na Utaratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.