Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu utakuwa katika maeneo yafuatayo:-
Kwanza, mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Umma. Serikali ihakikishe kwamba waajiriwa wote katika Utumishi wa Umma wanapoajiriwa kwa mara ya kwanza wanapatiwa mafunzo elekezi katika maeneo mbalimbali kama vile, uwajibikaji, maadili, OPRAS, Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali. Bajeti ya mafunzo ipelekwe Utumishi ili Chuo cha Utumishi kitoe mafunzo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile viongozi wanaoteuliwa katika ngazi mbalimbali wapewe induction na orientation ya majukumu yao ya kusimamia rasilimali watu, fedha na mali za Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ni suala la OPRAS, lazima ifike mahali Serikali kuanza kuwachukulia hatua watumishi ambao hawajazi fomu za OPRAS. Pia Taasisi zisizofanya vizuri na zinazofanya vizuri, katika kutekeleza OPRAS zitangazwe hadharani ili wananchi wote wajue. Sanjari na hilo vigezo vya kupima taasisi mbalimbali vitayarishwe na kuanza kutumika.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, ni fedha za TASAF awamu ya tatu katika baadhi ya maeneo; fedha hizi zinalipwa kwa wasiohusika kama pale Vwawa Mjini na baadhi ya vijiji, hebu fanyeni uchambuzi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, nnem ni usimamizi wa malipo ya mishahara; kuna haja ya kuongeza jitihada za kusimamia mfumo wa mishahara (Lawson version 9), bado Watumishi hawaitumii sawa na kusababisha ucheleweshaji wa malipo kwa baadhi ya watumishi. Waajiriwa wapya ni waathirika sana wa hili. Pia watu wanaoachishwa kazi na kustaafu kazini.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tano, ni kuboresha miundo ya Utumishi katika Kada mbalimbali. Hivi sasa miundo ya Kada nyingi imepitwa na wakati, lini mtaanza kuipitia upya miundo hiyo? Pia taasisi nyingi zimekuwa zinaanzishwa bila kuwa na miundo ya Taasisi husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la sita, ni kuhusu Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania. Kwa kuwa, Chuo hiki kilianzishwa ili kutoa mafunzo ya Uongozi, Menejimenti na Utawala Serikalini, je, ni lini hasa Serikali itaanza kukitumia Chuo hiki ipasavyo ili kitoe mchango unaohitajika katika kujenga rasimali watu iliyotukuka. Sanjari na hilo Chuo kinategemea kufundisha Watumishi wa Umma wangapi katika mwaka wa fedha 2016/2017. Pia ningependa kujua tafiti ngapi na katika maeneo yapi chuo kimepanga kufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.