Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Azza Hilal Hamad

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kupata nafasi hii ili nitoe mawazo yangu katika Wizara hii ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara hii iangalie suala la maji upande wa mifugo yetu. Tunaishukuru Serikali yetu ya Awamu ya Tano kwa mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria ambao utatoka Solwa – Tinde – Nzega – Igunga
– Tabora na maeneo mengine. Naomba Wizara itambue kwamba matumizi ya maji si kwa binadamu tu, ni nyema wakajenga mabirika kwa ajili ya kunyweshea mifugo yetu ili tatizo la maji lipungue au liishe kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Wizara ya Kilimo izingatie mradi wa umwagiliaji wa Kijiji cha Ishololo katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga. Serikali imetumia fedha nyingi katika mradi huu lakini hauna tija kwa kuwa ndani ya mwaka mmoja tuta lilishabomoka na hivyo kufanya bwawa hilo kutokuhifadhi maji kama ilivyokusudiwa. Hata hivyo mkandarasi aliyefanya kazi hiyo ameacha mashimo mengi katika eneo hilo la bwawa na kuonekana kama uchafu na ni hatari kwa watoto wadogo hata watu wazima pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naunga mkono hoja.