Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii kwa muda mrefu inabadili matamko kuhusu kilimo, lakini hakuna tamko hata moja lililofanikiwa katika kuboresha kilimo na kuleta matokeo chanya. Kwa mfano pamoja na Serikali kusema Mkoa wa Morogoro ni ghala la chakula, lakini ukifuatilia kwenye mkoa huo hakuna jitihada za makusudi za kuufanya mkoa huo kuwa ghala la chakula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshindwa kumaliza tatizo la wakulima na wafugaji, kuboresha upatikanaji wa pembejeo, kuajiri wagani hasa Jimbo la Mlimba ambapo hali ya wataalam wa kilimo na mifugo ngazi za kata hakuna. Kwa hali hii kilimo kitakuwaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu soko la mchele Serikali kwa miaka yote hamumtendei haki mkulima wa mpunga na kumuacha mkulima kutokuwa na soko la uhakika na kumuongezea umaskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itilie mkazo uanzishaji wa mabwawa ya samaki ili kuboresha maisha ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.