Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ina mpango mzuri lakini fedha inayotengwa kwenye Wizara ni ndogo mara zote na wakati wote fedha ya ndani ni ndogo zaidi. Fedha ya nje ni kubwa kidogo. Vilevile fedha inayopatikana kwenye bajeti zinazotengwa ni fedha kidogo sana na mara nyingine fedha ya nje inatolewa nyingi kidogo kuliko ya ndani. Maana yake ni kwamba kama Taifa tunaiacha sekta muhimu kuipa umuhimu wake, tunategemea wafadhili ambao wangependa kuona uchumi wetu hautengemai ili tubaki tegemezi kwa kila jambo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa kama ni mazoea kuwa kila mwaka pembejeo huwafikia wakulima kwa kuchelewa. Je, ni matarajio yapi yanayokusudiwa kuleta mapinduzi ya kilimo kwa utaratibu huu? Naomba Serikali itusaidie namna ya kumaliza kabisa tatizo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa yapo makampuni yanayojitangaza kuzalisha na kusambaza mbegu na dawa mbalimbali za kilimo, mengi yanakuwa fake na hakuna hatua zinachukuliwa hasa kwa dawa za kuua wadudu na palizi (kuuwa magugu).

Mheshimiwa Mwenyekiti, Programu ya Kuboresha Kilimo (ASDP) inayokuwa na malengo ya kuongeza tija kwa mkulima, kuongeza uzalishaji ili kuhuisha viwanda, kuwezesha mkulima wa chini, kuongeza kipato na kuongeza thamani ya mazao ili wakulima na kilimo kwa ujumla kiwe ni kazi yenye kuleta manufaa makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iratibu katika mpango huu kuboresha barabara katika maeneo ya uzalishaji katika Jimbo la Nkasi Kusini. Barabara zifuatazo ni muhimu kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo, nazo ni barabara ya Milundikwa – Kisu - Malongwe ni muhimu kwa kilimo Jimboni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kasu – Katani – Myula ni muhimu sana kwa maendeleo ya kilimo Wilayani. Vilevile barabara ya Nkomo II – Kipende, nayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Nkasi Kusini tuna mabonde mawili yanayofaa kwa umwagiliaji, nayo ni Bonde la Kate lenye hekta 1,500 na Bonde la Namansi lenye ukubwa wa hekta 440. Mabonde yote yameombewa fedha na Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi lakini bado kupata fedha ya kuanza kujenga miundombinu ya kumwagilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ranchi ya Karambo ina ukubwa wa hekta za eneo 23,000 lina ng’ombe 710 tu, kondoo 215, farasi nane, uwezo wake ni ng’ombe 7,000. Under-utilized.

Mheshimiwa Mwenyekiti, please Serikali iongeze mtaji.