Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuchangia hotuba ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Kilimo ni uti wa mgongo. Katika nchi yetu asilimia 75 tunategemea kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sekta ya Kilimo ni muhimu ila inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinaathiri ukuaji wake. Kwanza, ni utoaji mdogo wa fedha za bajeti ya maendeleo, upungufu mkubwa wa Maafisa Ugani, wataalam wa utafiti na upungufu wa kuchakata bidhaa zake. Kubadilika kwa tabianchi inaathiri kilimo kama vile kupata ukame, mimea kupata ugonjwa, mvua zisizotabirika, mashamba kupoteza ubora wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iwaangalie wakulima wadogo wadogo kwa kuinua juu mazao yao. Wakulima wanapata hasara kutokana na mazao yao kukosa soko la uhakika. Leo utaona mazao mengi yanaharibika, mfano, mananasi, embe, machungwa, nyanya na pesheni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii inawarudisha nyuma wakulima na kumrudisha kwenye umaskini kwa sababu itambidi lazima auze mazao yake kwa hasara. Je, Serikali ina mkakati gani wa kumwinua mkulima ili aweze kurudisha angalau hasara ya nguvu zake (mbolea).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uvuvi ambao unainua pato la nchi yetu kwa biashara na pia kuwainua wananchi kimapato katika maisha ya kila siku. Pia samaki ni chakula chetu na kila mtu anahitaji kula samaki ili kupata protein nyingi na kujenga afya yake. Sekta hii imemezwa na Sekta ya Viwanda. Tunahitaji tupate viwanda vingi vya kusindika samaki ili kupata tija zaidi. Viwanda vyetu vilivyokufa vinahitaji vifufuliwe na vifanye kazi. Samaki wapo wengi, tutakula na wengine tutainua biashara kwa ukubwa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji viwanda katika Ukanda wa Pwani kwa mfano Dar es Salaam, Tanga, Lindi, Mtwara Mafia, Zanzibar na Pemba. Samaki hawa wakivuliwa na kusindikwa, wengi watapata ajira na Serikali itapata kodi mbalimbali na itainua uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni nchi ya tatu Afrika kwa kuwa na mifugo mingi ukilinganisha na nchi kama Ethiopia na Botswana. Pia ng’ombe hutoa maziwa mengi lakini tunashindwa kusindika. Tunahitaji kujenga viwanda vingi tukamwinue mfugaji na pia tukainua uchumi wa nchi yetu kwa kusafirisha maziwa ya kopo tuachane na kuagiza kutoka nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina haja ya kuwapa elimu kubwa wafugaji kuhusu kuitunza ngozi na kuzikausha vizuri ili apate bei nzuri ili apate kujua tija ya kazi yake. Mfano, Ethiopia inafaidika kupata dola milioni 186 kwa mwaka 2016 kwa uzalishaji wa biashara ya ngozi pekee. Je, Serikali yetu inaingiza shilingi ngapi kwa mwaka kwa biashara ya ngozi pekee?

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mchango wangu, naomba kuwasilisha.