Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipate orodha ya wawekezaji wenye vitalu vya kufuga ng’ombe katika ranchi ya Misenyi. Nitashukuru sana nikipata orodha yao ikibainisha na uraia wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko taarifa kwamba wafugaji wengi wanaofuga ng’ombe Misenyi ranchi haijulikani wanakouza ng’ombe wao. Je, Serikali inazo taarifa kuhusiana na jambo hili? Kwa mwaka ng’ombe wangapi wanauzwa Misenyi ranchi na nani ni wanunuzi wakuu? Pia je, Serikali inatumia shilingi ngapi kupambana na magonjwa yanayosumbua ng’ombe katika ranchi ya Misenyi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ufugaji wa samaki Ziwa Victoria unazinufaisha sana nchi jirani isipokuwa Tanzania. Kwa upande wa Tanzania mfugaji wa samaki akitaka kufuga samaki Ziwa Victoria anatakiwa kufanya nini? Hapa Tanzania kwa hivi sasa tunao wafugaji wangapi wa samaki katika Ziwa Victoria? Je, kuna samaki ambao hivi sasa wamepotea au kutoendelea kupatikana katika Ziwa Victoria? Samaki hao kama wapo ni aina gani? Tanzania tuna mpango gani wa kuhakikisha chakula cha samaki cha viwandani kinapatikana kwa gharama nafuu na je Tanzania tuna viwanda vingapi vinavyozalisha chakula cha samaki?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.