Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani kwa sababu imeonesha namna gani ya kuboresha na kutatua kero zilizopo katika Wizara hii hususan wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya wakulima na wafugaji ni migogoro inayosababishwa na Serikali kwa wafugaji. Naomba Serikali itatue kero na mapigano yanayoendelea katika makundi haya mawili. Serikali ina uwezo kabisa wa kutatua migogoro hii? Nini kifanyike? Serikali itenge maeneo maalum kwa wafugaji na wawe wanalipia maeneo hayo. Wakulima wapewe maeneo rasmi ili kuondoa vita hii kati ya wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali isifanye siasa na makundi haya mawili. Tutabaki na Tanzania ambayo ni jangwa, wakati huo huo njaa kwa sababu kila eneo wakulima/wafugaji watafanya shughuli zao bila kujali utunzaji wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi. Serikali isifanye siasa kwa kuongea tu bila utekelezaji. Ihakiki maeneo ili wafugaji wasiingilie mashamba na kuharibu mazao ya wakulima lakini pia wakulima nao Serikali ikipanga eneo la malisho basi wakulima wasilime kila eneo ili kutatua hii migogoro ya mapigano na vita kati ya makundi mawili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Katavi – Wilaya ya Tanganyika na Mlele ni moja ya maeneo yaliyopita katika migogoro mingi na Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Operation tokomeza ujangili, operation kuondoa wavamizi wa maeneo ya wakulima na wafugaji. Kata ya Kabage Wilaya ya Tanganyika, Mwampuli, Chemalendi, Mgimoto, wafugaji waliondolewa na Serikali kwa kupigwa, akinamama kubakwa na Askari wa Wanyamapori, wakaibiwa pesa zao, kuibiwa mali zao madukani. Je, hili lilikuwa lengo la Serikali kuwanyanyasa wananchi katika Kata ya Isengule, maeneo ya Lyamgoloka kuchomewa nyumba na Askari hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka leo Serikali haijawahi kuwafidia wananchi waliokumbwa na kadhia hii. Walipwe fidia, Askari waliohusika kufanya vitendo hivi wapo na wanatembea kifua mbele huku wafugaji wakifilisika katika Taifa lao. Wananchi wakielezwa mipaka yao nadhani migogoro itapungua kuhusu utunzaji mazingira, kuhusu mipaka yao katika kilimo na ufugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vifo vya wafugaji, wafugaji wanapigwa risasi, ng’ombe wanaibiwa na hawa Askari. Je, Serikali ina lengo la kuwamaliza wafugaji, kwani ni dhambi mtu kuwa na mifugo mingi, Serikali iweke mkakati wa viwanda ili kupunguza migogoro hii wafugaji, visindike nyama na masoko yapatikane wananchi/wafugaji wakipata faida katika masoko kelele zitapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katavi na Vyama vya Ushirika. Katika hotuba hii nimeona Katavi kuna vyama vya msingi vya ushirika 14, wakati Mikoa mingine viko zaidi ya elfu moja. Je, hamuoni Katavi hamuwatendei haki? Katika vyama vya msingi ushirika vilivyopo pia kuna wizi wa waziwazi kwa wakulima wa tumbaku, zaidi ya milioni 600 zimeliwa na Viongozi Nsimbo- Katavi.