Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nianze kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri wanayoifanya. Niwapongeze Waheshimiwa Mawaziri, ni wazee lakini ni vijana kwa sababu wametembelea karibu miradi yote ya nchi yetu ya Tanzania. Niwapongeze watumishi wakiongozwa na Katibu Mkuu kwa kazi nzuri wanayoifanya. Niwapongeze Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi wanayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wetu wa Simiyu tumeweza kufanikiwa Mradi wa Ziwa Victoria utakaogharimu Euro milioni 300. Mradi huo utavinufaisha vijiji 253, lakini katika Jimbo langu la Itilima vijiji 64 vitanufaika na mradi huo.

Niiombe Serikali, hususan suala la wakandarasi ambao wanatekeleza miradi katika maeneo yetu iweze kuweka kipaumbele pale certificate Halmashauri zinazopeleka kwenye Wizara, waweze kulipa haraka ili shughuli hizi ziweze kufanyika kwa ufanisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua fedha ni kidogo, lakini fedha hii iliyotengwa inaweza ikafanya kazi, hususan pale ambapo itakapotoka. Pia niiombe Serikali iweze kupokea ushauri na mapendekezo tuliyoyatoa, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Maji kwa kutambua kwamba, fedha hizo zitakazotokana na maji na ndizo hizo sasa zinazoweza kufikisha asilimia 19.8 ya miradi inayoendelea hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo niiombe Wizara, pale kwenye suala la upangaji wa bei katika miji ambayo wanakuwa wamekamilisha miradi, katika sheria yetu inachukua siku 45, tumefanya ziara tumekutana na malalamiko mengi kwa wananchi kwamba inachukua muda mrefu na kusababisha kufanya vurugu katika baadhi ya maeneo. Kwa hiyo, niiombe Serikali pale ambapo wanakuwa wamekamilisha waweze kufanya utaratibu wa haraka zaidi hususan kwenye eneo la EWURA, kutoa bei elekezi ili wananchi katika maeneo hayo waweze kupata maji yenye bei salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuendana na udhibiti wa mapato katika nchi yetu niiombe Serikali iweze kufanya utaratibu wa kufanya kama mfumo wa vocha hasa kwenye miji mikubwa ambayo inaendelea kukua ili tuondokane na suala la maji kuwakatia wananchi. Pale ambapo mwananchi atakapokuwa na bili zake na kadi yake atakuwa anajiongoza kulingana na mapato yake na utumiaji wa maji katika maeneo yake. Tukifanya hivyo tutakuwa tumepunguza lawama na tutakuwa tumeipunguzia Wizara majukumu ya kupambana na suala la ukataji wamaji bila sababu. Maji yake yale atakayokuwa ameyalipia ndiyo yatakayofanyakazi katika nyumba yake na sehemu nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kuipongeza Wizara, katika Wilaya yangu ya Itilima nilikuwa na mabwawa 17, lakini mabwawa 6 tayari nimeshapata fedha na shughuli zinaendelea kupitia Mkandarasi DDCA. Niiombe tu Serikali iendelee kujenga uwezo katika Kampuni ya Serikali DDCA ambayo inafanya kazi nzuri na inawaridhisha Watanzania hususan watu wa Itilima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hayo niendelee kuiomba Serikali katika mji wetu wa Bariadi, kwa maana ya kwako Mheshimiwa Mtemi Chenge, pale Somanda kuna tenki kubwa limejengwa lenye uwezo wa kubeba lita 65,000 pamoja na Sima, mji ule unakua kwa kasi. Niiombe Serikali pia iweze kutilia mkazo eneo lile liweze kupata maji safi na salama, ili wananchi wa Mkoa wa Simiyu waweze kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee tu kuipongeza Wizara, niwapongeze Mawaziri, kazi ni ngumu. Watanzania wote tunahitaji kung’aa, lakini tunawategemea ninyi. Pamoja na kwamba ni wazee, lakini ni vijana ambao mmeaminika katika Taifa hili muweze kufanya kazi ambayo italeta tija katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana.