Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Spika naomba kuchangia kwa kushauri mambo yafuatayo:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, Serikali isaidie ujenzi wa ofisi ya Tume ya Maadili, wasaidiwe vyombo vya usafiri angalau gari moja kila mwaka, ikibidi wakope kwenye Mifuko wajenge na Serikali ilipe polepole ili waache kupanga kama sehemu ya kupunguza gharama kwa Serikali pia kama sehemu ya kutunza siri na ulinzi wa kutosha kwenye ofisi zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, ni kuhusu Ofisi ya Nyaraka za Serikali. Hiki ni kitengo muhimu sana naomba wapewe fedha kwa awamu, pia wajenge na kwa sababu wana maeneo wasaidiwe. Watumishi kwenye Wilaya na Mikoa huonesha uzembe mkubwa katika utunzaji wa nyaraka katika maeneo yao, nashauri watumishi wazembe kupitia DED watambuliwe na kupewa onyo kali.