Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nachukua fursa hii kwanza kupata nafasi hii. Niishukuru Wizara kwa kuwasilisha bajeti hii ya mwaka huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kwa haraka haraka nilitaka kuzungumza mambo mawili, moja, suala zima la bajeti. Ni kweli bajeti imeshuka lakini bajeti iliyokuwepo ndio uhalisia. Si vema kuwa na bajeti kubwa isiyoweza kufikia malengo, ni vema kuwa na bajeti ambayo kweli tutaweza kuisimamia na kuweza kupata kile ambacho tulichokuwa tumekikusudia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niungane na wenzangu wote kuitaka Serikali kwamba suala la shilingi 100 katika Mfuko wa Maji hili si la kuweka kigugumizi, kwa sababu imekuwa ni kila siku, suala hili limezungumzwa sana mwaka wa jana. Kama fedha hizi zingelipatikana tungelikuwa na zaidi ya shilingi bilioni mia tatu na sitini kwa mwaka na miradi mingi ingeweza kutekelezeka mbali na kutegemea fedha kutoka Serikalini moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti ,kwa hiyo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge wenzangu tuungane, kwa hili suala la shilingi 100 kama Serikali haitakubali kuongeza basi tuchukue hatua zinazofaa; kwa sababu Serikali haliigharimu chochote, Serikali ni kukubali tu shilingi 100 zikatwe kwenye mafuta, haina gharama yoyote. Niiombe sana Serikali hapa ilizingatie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili tunakabiliwa na changamoto kubwa ya uzalishaji wa mazao mbalimbali kupitia kilimo cha irrigation. Kwenye eneo la irrigation fedha hazikwenda kabisa. Tuna miradi mingi na maeneo mengi ya Tanzania tunahitaji tuweze kuwa na kilimo cha umwagiliaji maji. Mimi langu ni kutoa rai kwa Serikali na Wizara hii na hasa Makatibu Wakuu na Kamisheni ya Umwagliaji Maji tuzingatie rai nitakayoitoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo langu mimi nilisema tokea kipindi kile cha nyuma kwamba Mfuko wa Umwagiiaji Maji ufufuliwe. Upo siku nyingi lakini hauna fedha hata shilingi, hautengewi fedha. Nilitoa wazo kwamba fedha hizi sisi tunaweza kuzipata kupitia mashirika ya simu. Tukatoa tu kiwango cha watu milioni 20 ambao wanamiliki simu hapa Tanzania wakikatwa shilingi 100 tu kila muamala wa shilingi 1,000 kwa siku 30 tu unazalisha zaidi shilingi bilioni 600.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha hizi tayari unaweza kutengeneza zaidi ya hekta 2400; hekta ambazo zitaweza kukuzalishia zaidi ya tani 330,060 kwa mwaka kama wakulima wataweza kulima mara mbili, kiwango ambacho kwa kweli ni full security ya nchi hii. Lakini ni chanzo cha uzalishaji wa viwanda mbalimbali katika nchi yetu. Tatizo letu liko wapi? Wenzetu wengine wametoa mawazo hapa wamesema watu wanakunywa bia kwa wingi, kwa nini tusikate shilingi 100 au shilingi 200 tukaweza kufufua huu mfuko na tukaweza kupunguza matatizo ya ukame na ukosefu wa maji katika maeneo yetu mbalimbali kwenye uzalishaji? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali tuzingatie haya, mengine tutakuwa tunapiga tu blabla kwa kusema kwamba tupate fedha moja kwa moja kutoka Serikali kuingizwa kwenye umwagiliaji maji si rahisi. Tuangalie Mifuko ya NSSF, PPF na mashirika mengine tukate kiwango kidogo kidogo. Mimi nimetoa mfano mdogo kwa siku 30 tu watu wangapi wanatumia shilingi 1,000 kwa miamala ya simu?

Tukifanya miezi sita nchi yote hii tumeifanya kuwa umwagialiji maji na tutakuwa na uhakika wa uzalishaji wa chakula nchini mwetu na ile dhana nzima ya Tanzania ya viwanda itatimia kupitia huko. Nafikiri tufunue mawazo tuangalie kwa upana zaidi kuliko hali ilivyo sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine nilichokuwa nimekiomba ni kwamba Serikali iangalie maeneo yale kame zaidi. Wazo la kuwasaidia hasa wafugaji katika maeneo mbalimbali kuepusha ile wanaita migration, movement ya wanyama kutoka eneo moja kwenda lingine kwa ukosefu wa maji. Suala la ujengaji wa mabwawa katika maeneo mbalimbali ndilo mkombozi wa suala hili, na litaunguza sana migogoro ya wafugaji na... (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Rehani.