Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuweza kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie fursa hii kumshukuru kwa dhati kabisa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa initiative na kusukuma Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria ambao sisi wakazi wa Mkoa wa Tabora tumekuwa tukiusubiri kwa muda mrefu. Nimshukuru kwa dhati kabisa Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu ambao tulishiriki pamoja pale Tabora katika sherehe ya kutia saini mkataba, na kwa taarifa zilizopo ni kwamba mwezi ujao wakandarasi wataanza kazi na kwa sisi tunaochunguza chunguza tayari zile Kampuni za Kihindi zimeshaonekana maeneo ya Solwa kule wakianza kufanya fanya shughuli za awali. Kwa hiyo, nishukuru kwa dhati kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nzega nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kuanza kutekeleza ahadi ya Rais ya shilingi milioni 200 ambayo ni fedha za awali kwa ajili ya kuondoa tatizo la maji wakati tunasubiri mradi huu wa miezi 36. Sasa hivi Nzega angalau tumeanza kupata maji kwa mgao kwa wiki mara mbili. Mwanzo tulikuwa hatupati, angalau kwa mwezi walikuwa wanapata mara moja. Lakini sasa hvi ime-improve two hundred. Nikuombe Mheshimiwa Waziri utakapokuja kuhitimisha ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati anakwenda Christimas ile milioni 200 iliyobaki inafiki lini Nzega? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme jambo moja, pamoja na shukrani zote hizi za dhati, niseme jambo la kusikitisha. Leo Nzega tuna siku tano hatuna maji na sababu ni moja tu, Mamlaka ya Maji ya Nzega ambayo imeanzishwa mwaka mmoja uliopita imekatiwa umeme na Shirika la TANESCO kwa sababu ya deni la shilingi milioni 206 ambalo chanzo chake ni Serikali Kuu kutokupeleka fedha za OC kwa zaidi ya miaka mitano, wananchi wanaadhibiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Bunge hili ningeomba, tunamnyooshea kidole Waziri wa Maji, jukumu na matatizo ya maji haya cause route ya haya yote tunayoyajadili ni Ministry of Finance. This is a biggest problem, kila sehemu tatizo fedha hazijaenda za maendeleo. Nataka niwape mfano mdogo, mimi natoka Kamati ya Huduma za Jamii, tuna matatizo ya x-ray kutokuwa serviced kwa sababu ya deni la Philips. Who is the problem? Ministry of Finance hawajamlipa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Mamlaka za Maji za nchi nzima zinadaiwa shilingi bilioni nane na Shirika la Umeme, lakini mamlaka hizi kwa ujumla wake zinadai taasisi za Serikali shilingi bilioni 39. Watanzania wanalipa bills zao tunawakatia maji kwa sababu taasisi za Serikali Kuu hazijalipa umeme. Anayeadhibiwa ni common man on the street. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo Katiba ya Chama changu hapa. Moja ya dhumuni, wajibu wa mwanachama, Wajibu Namba Tatu; “Kujitolea nafasi yake, kuondosha umaskini, ujinga, maradhi na dhuluma na kwa jumla kushirikiana na wananchi wote katika kujenga nchi yetu.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitakuwa sehemu ya dhuluma ya wananchi wa Nzega kukosa maji kwa uzembe unaotokana na maamuzi ya Serikalini, I will never be part of this. Sitaunga mkono Bajeti ya Serikali kwa sababu moja tu, Waziri wa Fedha aje hapa atuambie Waheshimiwa Wabunge anamalizaje deni la TANESCO ili Mamlaka za Maji zisikatiwe umeme kwa uzembe unaotokana na Serikali Kuu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge hapa tumejadili sana kuongeza fedha na mimi nashukuru Waziri wa Fedha popote alipo apigiwe simu au Naibu wake atuhakikishie hapa kwenye Finance Bill wanaongeza tozo la shilingi 50… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)