Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Makame Mashaka Foum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MAKAME MASHAKA FOUM: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kunijaalia kuwepo hapa na kutoa mchango wangu. Pia nawashukuru wananchi wa Jimboni kwangu kupitia Chama cha Mapinduzi kwa kunichagua kuwa Mbunge wao.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoendelea, hivyo bado tutakuwa na mahitaji makubwa ya uchumi na huduma za jamii kama vile upungufu wa hospitali za Wilaya, shule za Msingi na Sekondari. Pia tutakuwa na upungufu wa miundombinu kama barabara na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba hasa Vyama vya Upinzani pamoja na wananchi wote kuunga mkono Serikali hii inayoongozwa na Rais mpendwa, Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, Rais ambaye amedhamiria kwa dhati kuifikisha Tanzania kufikia uchumi wa kati.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili tufikie uchumi wa kati ni lazima kuunga mkono uchumi wa viwanda. Naishauri Serikali kuwa viwanda viwekwe kwa kuzingatia vipaumbele tulivyonavyo mfano, sehemu yenye wafugaji wengi wa ng‟ombe viwekwe viwanda vinavyotumia malighafi hiyo, vivyo hivyo sehemu yenye kuzalisha pamba kwa wingi viwekwe viwanda vyenye kutumia malighafi hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu ni nchi ya Dunia ya Tatu, naunga mkono uamuzi wa kuchukua miradi kidogo yenye kutekelezeka. Hali hii itatusaidia kupiga hatua nzuri ya maendeleo. Upo usemi usemao haba na haba hujaza kibaba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Mfuko wa TASAF wako wajanja huingia katika Mifuko hii na kupewa, nashauri Serikali za Vijiji ziwe makini ili kuzuia wajanja wasipate fursa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.