Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kuchukua fursa hii kumshukuru Mungu kwa kupata nafasi hii, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri ya kusimamia na kuliongoza Taifa hili kwa speed inayotakiwa. Nimshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa uteuzi wa Profesa Kitila Mkumbo, ninahakika akiungana na wenzake pale wanaweza kufanya kazi kubwa sana ya kusukuma nchi hii mbele pamoja na vijana wadogo wakina Luhemeja ambao sasa hivi wamepata nafasi ya kushughulikia matatizo ya maji katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ambayo wanaifanya Wizara ni kazi nzuri sana, lakini kuna baadhi ya mambo wanakutana hapa na upinzani mkubwa hasa wa takwimu zao, mimi nadhani wanatakiwa vilevile kufanya vile vile kazi ya RITA ya kusajili vizazi na vifo. Wanatakiwa wasajili visima vilivyokufa na vilivyo hai. Pengine kwenye orodha, wana orodha ya visima lakini vimeshapigwa radi siku nyingi vingine vimepigwa tetemeko wao kwenye vitabu wameandika kwamba visima vinatoa maji. Watajikuta wanapata matatizo makubwa bila sababu za msingi, sajilini takwimu za visima ambavyo havifanyi kazi na vinavyofanya kazi, mtapata kwa uhakika kwamba maji yapo kwa kiasi gani si kuleta tu kwamba kuna visima kadhaa na maeneo kadhaa yanapata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata visima vya zamani ambavyo vimekufa Halmashauri hazina uwezo wa kuvifufua. Kuna baadhi ya maeneo walikuwa na maji sasa hivi hawana maji. Kwa mfano ukija kutazama kwenye Jimbo la Mtera kuna Kata kadhaa zinahangaika kupata maji. Kata ya Handali, ukienda kutembelea Idifu, ukienda kutembelea Mlowa Bwawani wote hawana maji lakini ukija hapa unakuta takwimu vijijini ni 72. Kwa hiyo, nina uhakika wakisajili visima vilivyo hai na vilivyokufa wanaweza wakaja na mahesabu ya uhakika. Lakini nchi hii tuigawe kwenye vipande, kuna baadhi ya maeneo yanasubiri muda mrefu sana kupata huduma hii, tujue tu kwamba tutapata lini, nayo tukijua hiyo inaweza kutusaidia. Tumeona kuna ongezeko kubwa sana la huduma za maji mijini tumekubali na sisi tunayaona lakini kuna baadhi ya maeneo hata wananchi waelewe tu kwamba mwaka gani basi hii huduma muhimu ya maji itawafikia vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Maji ni Wizara mtambuka sana, na nashangaa tunapoijadili Wizara hii halafu Wizara ya Fedha haina Waziri wala Naibu Waziri humu ndani ya Bunge, hii si sawa. Ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliwaweka wawili mmoja akiwa hayupo mwingine yupo, hii ni dharau kubwa sana kwa Bunge lako Tukufu. Kwa hiyo, tungependa, tunapojadili Wizara muhimu kama hizi Mawaziri wa fedha wawepo, Bunge maana yake karibu ni Wizara tatu tu; ni kiti cha Spika, Waziri Mkuu na Waziri wa Fedha maana humu tunazungumzia hela sasa tukiwa tunazungumzia pesa wahusika wa fedha hawamo kidogo inatupa matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vitu hapa vinazungumzwa, jana kulikuwa na Mbunge mmoja alikuwa anaicheka Serikali na kuibeza kwanini Rais ameanza na ndege asianze na maji. Jamani, nataka leo nitoe somo kidogo hapa. Ndege ni sawa sawa na mkulima mwenye kilo moja ya mahindi ndani hana chakula na mvua zimeanza kunyesha, anatakiwa achague akaange ile kilo moja afe au apande apate mahindi mengi ili aweze kuishi? Mheshimiwa Rais alipoleta ndege ameleta biashara ili izalishe tupate hela za kutengeneza maji mengi zaidi, kwa hiyo, badala ya kumbeza tumuunge mkono,Waheshimiwa Wabunge tumuunge mkono Mheshimiwa Rais, nchi haiendeshwi kwa hapana.

Nataka niwambie, kwamba duniani kuna aina tatu za upinzani; uko uoinzani shinikizo wanashinikiza hoja, upo upinzani kioo na uko upinzani serious, huu wa Tanzania ni upinzani kioo. Kama hujachana wanakwambia hujachana kesi inaisha unaendelea na shughuli zako. Kwa hiyo, Serikali msiwe na wasiwasi tuendelee kujipanga kufanya kazi za maendeleo ya nchi hii, tusishughulike na upinzani kioo ambao kaa hawajachana wanakwambia umechana kasoro Zitto tu ndiyo anajitahidi na kwa sababu yuko peke yake. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi umeona walivyomuabisha Makamu Mwenyekiti wa Chama, amekuja Profesa Safari kugombea hapa amepewa kura 30 na hawa, hawamtaki Makamu Mwenyekiti wa Chama chao awe kiongozi, hawa ndiyo wanaweza kupewa Serikali, haiwezekani watu ambao hawaheshimiani, haiwezekani. Kwa hiyo, nakushukuru sana, mimi naunga mkono hoja, lakini nawaambia Serikali msihofu upinzani tufanye kazi. Ahsante.