Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima tutafute tozo fulani kisha fedha hiyo izungushiwe (Ring Fencing) kama REA, vinginevyo tunajidanganya. Hali ya maji huko vijijini ni mbaya kuliko mnavyodhani. Ni aibu!

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Nyakalura uliigharimu Serikali shilingi bilioni moja lakini mpaka leo hakuna maji. Harufu ya rushwa kwenye mradi huo iko wazi, chukueni hatua, wananchi wanalalamika. Mji wa Kabindi unakua kwa kasi na sasa idadi ni takriban 25,000, hakuna maji kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.