Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji vya Jimbo la Mbozi vinakabiliwa na tatizo kubwa sana la maji. Baadhi ya Vijiji hivyo ni Iyenga, Ilea, Itumpi, Magamba, Mtunduru, Utambalila, Maninga, Mahenje na vijiji vinginevyo. Hivyo katika miradi ya maji vijijini ni vizuri Serikali ikavikumbuka na vijiji hivi vya Jimbo la Mbozi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji Mdogo wa Mlowo wenye idadi ya watu wasiopungua 60,000 unakabiliwa na tatizo sugu na la muda mrefu sana la maji. Bajeti ya mwaka uliopita 2016/2017, Mji Mdogo wa Mlowo ulitenga fedha kwa ajili ya maji. Kwa bahati mbaya na masikitiko makubwa sana, hadi sasa hakuna shughuli yoyote inayoendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri atatue tatizo la maji Mji Mdogo wa Mlowo kwani wananchi wanateseka sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, vipo vyanzo vingi vya maji Wilaya ya Mbozi mfano, Mto Lukululu, Mto Mkama na mito mingine. Ni vyema Serikali ijikite kuwapatia maji wananchi wa Mbozi kutoka katika vyanzo hivi. Pia maji ya ardhini hayapo mbali, maeneo mengi yanapatikana mita 75 kuelekea ardhini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.