Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza sana ushirikiano wa Wizara na Watendaji wake wanaonipatia wakati wote.


Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi hizi, naomba pia nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, Katibu Mkuu pamoja na Naibu Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara kwa miongozo wanayotupatia Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe. Naomba kutoa mchango wangu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe imeleta Wizarani maombi ya kupatiwa vibali vya kujenga miradi ya maji kwenye Wilaya yetu. Kwa mijini, tunaiomba Wizara iharakishe miradi ya Mji wa Ushirombo kwani Wilaya hii pamoja ukongwe wake haina mtandao wa maji mjini hasa kwenye Kata za Igulwa, Kateute, Bulaugwa na Ushirombo. Wananchi kama ilivyo kwenye maeneo mengine ya Wilaya, wanapata shida kubwa sana ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kata ya Uyovu tuna chanzo cha maji kikubwa ambacho kama kitapatiwa fedha, kinaweza kusambaza maji kwenye mji mdogo wa Runzewe ambako maeneo ya Kabuhima, Azimio, Kanembwa na baadhi ya maeneo ya Kabagale. Naiomba Wizara itusaidie kupata fedha kwa ajili ya kupanua mradi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya umwagiliaji iliyopo Bukombe imesimama muda mrefu. Mradi wa Nampangwe na Bugelenga imesimama. Pamoja na kutumia fedha nyingi za Serikali lakini fedha ya kukamilisha haijatolewa jambo ambalo hadi leo wananchi wanaona halina manufaa. Naomba miradi hii ipatiwe fedha ili ikamilike na wananchi wa maeneo haya waweze kulima kwa tija katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo haya yakipewa kipaumbele yataondoa kabisa tatizo la njaa kwenye Mkoa wa Geita na Mikoa ya jirani.