Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Maji ni uhai, kila chenye uhai kinahitaji maji. Hivyo napongeza juhudi kubwa inayochukuliwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi kupitia Wizara hii kwa jitihada ya kuwafikishia huduma hii wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mahitaji ya maji ni makubwa katika nchi yetu na tunashuhudia wakati huu wa mvua za masika maji mengi yanavyopotea, tunaiomba Wizara ya Maji iandae program mahususi ya kuvuna maji ya mvua ambayo kwa sasa yanapotea bure.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango mwingine ni kuwaelimisha wananchi au taasisi, mfano shule, vituo vya afya na kadhalika, wavune maji kupitia mapaa ya nyumba na kuyahifadhi. Kwa wafugaji wenye mifugo mingi waelimishwe kujiandalia mazingira yatayowezesha kuhifadhi maji hasa wakati wa mvua ambapo maji mengi hupotea bure.

Mheshimiwa Naibu Spika, akinamama kwa asilimia kubwa ndio wanaosumbuka na watoto wao kutafuta maji. Nashauri kuvitumia vikundi vya akinamama katika program mbalimbali za kuvuna maji na kuyahifadhi kwa matumizi endelevu. Tutumie na vikundi vya vijana kubuni njia nafuu za kuvuna maji kwa matumizi ya kilimo na mifugo katika kipindi hiki cha mvua, kwani maeneo mengi mvua zimefika kwa wingi na maji yanapotea bure.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii kwa kuongezea tozo kwenye mafuta ili kuongeza Mfuko wa Maji.