Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Vunjo maeneo mengi hayana maji safi na salama toshelezi. Mfano ni Kata za Mwika Kusini, Makuyuni, Kahe Mashariki, Kahe, Kirua Kusini, Kilema Kusini, Momba Kusini na Kirua Magharibi. Sehemu nyingine tajwa hapo juu, miundombinu ya maji ni ya zamani sana, ni chakavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Momba Kusini walishirikiana na Mbunge, wameanza utaratibu wa kitaalam wa kuwa na andiko ambalo linakadiria mahitaji ya takriban shilingi milioni 100.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tumekubaliana kila kaya kuchangia sh.10,000/= lakini chanzo cha fedha hizi hazitoshelezi. Je, Serikali itasaidia kiasi gani katika mradi huu kama kichocheo? Kutoka chanzo cha maji ya uhakika kimepatikana Kisumbe, Mamba (South Water Supply System from Kisumbe Spring). Nashauri elimu shirikishi kwa wananchi namna bora ya kuyatawala, kuvuna/kuyasimamia na kuyatumia maji.