Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Hata hivyo, nitoe ushauri ufuatao:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara/Serikali ije Bungeni na mpango mkakati (strategic plan) wa kuhifadhi vyanzo vya maji nchini. Nchi hii ina mito, maziwa na hata mabwawa madogo ya asili. Ni vizuri Serikali ikafikiria namna bora ya kuhifadhi vyanzo vya maji. Mfano, Mkoa wa Kigoma una vyanzo zaidi ya 1,000. Serikali ije na mpango shirikishi ambao utazishirikisha Mamlaka na Halmashauri zetu ili kutunza na kuhifadhi vyanzo vya maji ambavyo vinaharibiwa kwa kasi ya ajabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maji utakaofadhiliwa na Serikali ya India kwa USD 500, kati ya miji itakayonufaika na fedha hizo ni pamoja na Mji wa Kasulu. Nashauri sana process hii iharakishwe ili wananchi wetu wanufaike na huduma ya maji. Aidha, katika Mji wa Kasulu, maji yaliyopo/yanayotoka ni machafu na yamejaa tope. Tafadhali Wizara ije na mpango wa dharura kwa ajili ya maji katika Mji wa Kasulu. Maji ni machafu, Wizara chukueni hatua za dharura.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya maji ya muda mrefu katika Wilaya ya Kasulu iliyoanza miaka ya 1980, mfano Mradi wa Maji wa Ruhita (Ruhita Water Scheme 1984) ni mradi wa siku nyingi. Nashauri Wizara itume wataalam wa maji waende Wilaya ya Kasulu wasaidiane na Halmashauri ya Mji wa Kasulu (Kasulu TC) ili Miradi ya Maji ya Ruhata, Kanazi, Mrufiti na Msambara itazamwe upya hatimaye mkakati wa rehabilitation uanze/uandaliwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.