Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kufanya kazi kwa weledi mkubwa na kwa kuwa wasikivu kwa sisi Wabunge. Pongezi pia zimwendee Katibu Mkuu na watumishi wa Wizara kwa mipango yenye kuleta matumaini ya kumtua mama pamoja na watoto wetu ndoo vichwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kutenga $ 30m kwa ajili ya mradi wa Lwakajunju (Kayanga), Ukurasa wa 85 wa Hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Naomba Wizara ifanye hima mradi huu uende kwenye utekelezaji, kwani kiasi hicho hicho kilitengwa Financial Year 2016/2017, lakini hakukuwa na disbursement, same amount ime-carry forward Financial Year 2017/2018. Sasa naomba this time twende kwenye utekelezaji kwani mradi huu ndio uhai wa kura za Mheshimiwa Rais, Mbunge na CCM kwani ndiyo ilitusababishia ushindi 2015. Mradi huu naomba usifanye kosa la kushindwa kuacha huduma ya maji kwa vijiji vyenye chanzo (Lake Lwakajunju) yaani Kafunjo, Nyakashenyi, Kijumbura, Bweranyange, Kijumbura, kutasaidia ulinzi shirikishi kwa additional benefits.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara iliiomba Halmashauri ya Karagwe kuleta taarifa ya maeneo yenye uhaba mkubwa wa vyanzo vya maji. Rejea barua yenye Kumb Na. DE 208/ 287/OIN/96 ya tarehe 15/04/2016 na majibu ya hiyo barua Kumb Na. KGR/HWK/T.6/9.Vol.1/02 ya tarehe 22/04/2016. Vijiji hivi ni Nyakahita, Kigarama, Kashanda, Chonyonyo, Chabuhora na Kishoju. Naomba sana Wizara itusaidie kwenye utekelezaji wa bajeti iliyowasilishwa na Wizara. Aidha, naomba niongeze Kijiji cha Rwenkorongo nacho kina shida kubwa ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Nawapongeza tena kwa kazi nzuri na Mwenyezi Mungu awajalie afya njema. Ahsante.