Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi na mimi niweze kuchangia kwenye hoja hii muhimu iliyoletwa na Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Mheshimiwa Spika, tatizo la maji limekuwa ni changamoto kubwa kwa Taifa letu hususan, Mkoa wangu wa Iringa.

Mheshimiwa Naibu Spika, shida hii ya maji inamgusa mwanamke moja kwa moja. Wanawake wamekuwa wakipoteza muda mwingi kutafuta maji badala ya kujitafutia maendeleo yao ya kiuchumi. Tatizo hili la maji si tatizo mjini tu, bali vijijini nao wamesahaulika kwa muda mrefu. Ili nchi yetu iweze kufikia malengo ya Tanzania ya uchumi wa kati lazima tuhakikishe hii nguvu kazi (wanawake) ambao ndio wazalishaji wakubwa tunawaondolea adha hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niungane na Waheshimiwa Wabunge wenzangu, naomba tuongeze tozo ya sh.50 kwa lita, ili tuwe na chanzo chenye uhakika. Kama hii haitawezekana, basi tupunguze kwenye other sources kama Road Funds na REA. Nina imani kubwa na Serikali na Wizara kuwa watapokea ushauri wangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.