Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza uongozi wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya. Pongezi ziende kwa Waziri wa Maji Mheshimiwa Injinia Gerson Lwenge, Naibu Waziri Mheshimiwa Injinia Isack Kamwelwe, Katibu Mkuu Profesa Kitila Mkumbo na Naibu Katibu Mkuu Injinia Emmanuel Kalobelo.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo yangu ya uchangiaji ni kama ifuatavyo:-

Kwanza ni Wizara kupewa fedha za kutosha. Takwimu za mwaka jana zinaonyesha Wizara ilitengewe fedha za maendeleo shilingi bilioni 915.2, hadi Machi zimetolewa shilingi bilioni 181.2 sawa na asilimia 19.8. Hakuna miujiza kuwezesha Wizara hii kupata asilimia 80.2 zilizobaki. Tunasisitiza Hazina kutoa fedha kwa wakati kwa Wizara hii. Mwaka huu fedha za maendeleo zimetengwa shilingi bilioni 623.6, fedha ambazo ni pungufu ikilinganishwa na mwaka jana. Kufidia pengo hili nakubaliana na wazo la kuongeze tozo kutoka shilingi 50 hadi shilingi 100 kwa lita ya diesel na petrol.

Pili, miradi ya maji 17 ya AMREF. Kwa niaba ya wananchi wa Nanyamba napenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa kutoa fedha za kukarabati miradi ya maji iliyokuwa imejengwa kwa ufadhili wa AMREF, ukarabati unaendelea na Halmashauri Mji ilipokea shilingi milioni 400 ya awali. Ni matarajio yetu kuwa kiasi kilichobaki kitatoka mapema ili mkandarasi aweze kulipwa kwa wakati.

Tatu, ni kuhusu mradi wa maji wa Makonde. Mradi huu unahitaji ukarabati mkubwa, tunashakuru Serikali kwa kutenga fedha shilingi milioni 87.41 mkopo kutoka India. Ukurasa wa 62 wa kitabu cha bajeti imeelezwa utekelezaji unaanza mwaka huu lakini ukurasa 173 imeandikwa mradi wa Makonde upo Phase III. Hii maana yake nini? Wakati ukihitimisha Waziri atoe ufafanuzi kwa nini kuna maelezo ya kuwekwa Phase III mradi wa Makonde utapewa fedha baada ya kukamilika utekelezaji wa Phase I and II? Ufafanuzi unahitajika kuhusu utata huu unaotolewa na baadhi ya watendaji wa Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha nakumbusha Wizara kuhusu utekelezaji wa mradi wa maji kutoka Makonde na kupeleka kata vijiji 23 vya Halmashauri ya Mji Nanyamba. Andiko la awali limeshawasilishwa na usanifu wa mradi unaendelea.

Nne, mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma hadi Manispaa ya Mtwara Mikindani; mradi huu unatoa maji kijiji cha Mayembe chini kilichopo Halmashauri Mji ya Nanyamba na matarajio ni vijiji vyote vya jirani wapate maji, Mheshimiwa Naibu Waziri alifika hapa na kuahidi vijiji vya Mayemba Juu, Chawi na Kiromba, vijiji vilivyotajwa 26 ni vichache sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, nashauri Wizara iangalie uwezekano wa usanifu mradi mwingine wa kutoa maji Mto Ruvuma na kupeleka vijiji vya Halmashauri ya Mji Nanyamba. Kata za Kiromba, Kiyanga, Mtiririko, Mbembako na Kitaya wanaweza kupata maji kutoka Mto Ruvuma.