Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Rev. Dr. Getrude Pangalile Rwakatare

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. DKT. GERTRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwapongeze Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri mnayoifanya, tunashukuru kwa jitihada zenu zote japo bajeti hii ni finyu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niungane na Wabunge wenzangu kuomba nyongeza ya bajeti hiyo. Maji ni uhai, maji ni afya na maji ni viwanda. Kila taasisi inahitaji maji mashule,vyuo, hospitali na kadhalika, tunaomba Wizara hii muhimu ipewe kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishauri Wizara kuungana na Wabunge kupiga vita, wafugaji wanaonywesha mifugo yao kwenye vyanzo vya maji. Kwa mfano,Wilaya ya Kilombero ni bonde zuri kwa kilimo, lakini mifugo imesababisha mito kukauka, wakulima kunyanyasika na wageni wafugaji kwa sababu ya mifugo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Mfuko wa Maji Vijijini uanzishwe kama ilivyo kwenye umeme itasaidia sana.

Mwisho ninawapongeza sana kwa miradi mingi ya maji inayofanya vizuri sana, tunawaombea bajeti iongezwe ili mfanye vizuri zaidi.