Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, awali naomba niishukuru Serikali kwa hatua mbalimbali inazochukua kukabiliana na changamoto za upatikanaji wa maji nchini. Kimsingi naunga mkono mipango ya Serikali kupitia bajeti hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi naomba kuwasilisha maoni kwenye maeneo yafuatayo:-

Kwanza, scheme za umwagiliaji kutokuwepo Shinyanga; pamoja na ukweli kuwa Shinyanga ni kambi la njaa wakati mvua hunyesha na mabonde yanayofaa kwa umwagiliaji yapo, lakini cha ajabu ni kuwa katika mipango ya Serikali hakuna scheme hata moja katika bajeti. Jedwali Namba Nane, Shinyanga haipo kabisa, naomba maeneo yafuatayo yaingie katika mipango ya Serikali:-

(i) Sheme Bonde la Chela;

(ii) Scheme Bonde la Bumva; na

(iii) Scheme Mabonde ya Kashishi na Kabondo.

Pili, bili za umeme na ruzuku ya uendeshaji KASHWASA; kwa zaidi ya wiki mbili sasa Kahama na Shinyanga hakuna maji kwa sababu KASHWASA inadaiwa na TANESCO na hivyo umeme kukatwa. Naomba utaratibu wa utoaji ruzuku KASHWASA uangaliwe upya ili huduma za maji zisikosekane kwa wananchi wa Kahama na Shinyanga kwa sababu za Kiserikali wakati wateja wanalipa bili zao vema Tatu, mradi wa vijiji 100 vilivyoko pembezoni mwa Bonde la Ihelele - Kahama na Shinyanga ahadi ni ya muda mrefu tangu mwaka 2013 lakini kasi ya utekelezaji ni ndogo. Naomba mwaka huu angalau katika Jimbo la Msalala vijiji vya Mwakuzuka, Kabondo, Matinje, Izuga, Busangi, Nyamigege, Vula, Ntundu, Buchambaga, Mwaningi, Bubungu, Ntobo na Mwankima vipatiwe maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitashukuru kama maeneo haya yatazingatiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.