Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mungu kunipa afya na nguvu kuwatumikia wananchi Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania imejaliwa kuwa na maji mengi sana kutoka vyanzo mbalimbali kama maji juu ya ardhi, maji chini ya ardhi na maji ya mvua yanayosababisha mafuriko mara kwa mara. Hata hivyo, kila mara Tanzania imekuwa inakabiliwa na uhaba wa maji safi na salama katika maeneo mengi mjini na vijijini. Uhaba wa mvua unaosababisha ukame na kusababisha njaa na adha kubwa ya kiuchumi. Mfano, wanyama kufa na kukosekana kwa mazao, vilevile nchi imekuwa mhanga mkubwa wa mvua kubwa inayosababisha maafa ya mafuriko, uharibifu wa mazao na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, miaka 53 ya uhuru pamoja na wataalam waliobobea katika taaluma ya maji na mipango, Serikali imeshindwaje ku-manage suala la maji ili kupunguza kero na umaskini?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini Serikali haisimamii kwa Sheria ya Uvunaji wa Maji ya Mvua na Sheria ya Ujenzi irekebishwe kujumuisha miundombinu ya kuvuna maji kwenye majengo mbalimbali. Kwa nini mabwawa makubwa ya kukinga na kutunza maji kwenye maeneo ambayo kila mara kuna mafuriko na ya katumika kwa ajili ya kilimo, mazao na mboga mboga za muda mfupi ili kuinua uchumi wa wananchi na kupunguza umaskini?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini maeneo yenye maji chini ya ardhi wananchi wasichimbiwe visima ili kuwanusuru na kero ya maji? Katika hotuba, maeneo yenye maji chini ya ardhi yameainishwa, lakini hakuna popote fedha imetengwa kwa ajili ya kuchimba visima vichache kwa vipaumbele?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni rai yangu kwamba Wizara ijipange kukusanya/kuvuna maji mengi yanayopotea na kwenda baharini. Nchi ya Israel ni mahali pazuri pa kujifunza, maji ni almasi, hakuna tone linalopotea. Hapa kwetu tuna maji mengi lakini tunafanya mzaha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.