Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuwapongeza Waziri wa TAMISEMI na Waziri wa Utumishi kutoka Ofisi ya Rais kwa hotuba zao nzuri na jinsi wanavyochapa kazi. Pia nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri wa TAMISEMI, ndugu yangu Mheshimiwa Jafo anafanya kazi nzuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama kuchangia maeneo mawili. La kwanza upande wa michezo kwenye ngazi za chini kwa maana ya wilaya. Ilitokea hoja hapa ya namna ambavyo Wizara ya Michezo inaweza kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI katika kuimarisha michezo kwenye ngazi za chini. Tumeanza mazungumzo na wenzetu wa TAMISEMI tuone namna ambavyo taasisi zilizo chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo zinavyoweza kushirikiana na wenzetu wa local government katika kuhakikisha tunaboresha michezo katika ngazi hizo. Mfano mzuri wenzetu wa TFF sasa watashiriki katika mchezo wa mpira wa miguu kwenye UMITASHUMTA na UMISETA na hili liko mahali pazuri na tunakwenda vizuri. Kwa hiyo, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba safari hii michezo hii imeboreshwa sana. Tunaomba ushiriki wao katika kuhakikisha vijana wetu wanashiriki michezo hii vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili, ulifanyika utafiti hivi karibuni na ulifanywa na Waandishi wa Habari Wasiokuwa na Mipaka katika nchi 180 kuangalia uhuru wa vyombo vya habari katika nchi hizo. Matokeo ya utafiti huo yanaonesha kwamba katika hizo nchi 180 Tanzania ni nchi ya 71. Kwa hiyo, tunafanya vizuri sana duniani katika kuangalia na kutunza uhuru wa vyombo vya habari. Katika Afrika Tanzania ni nchi ya 11 kwa kutunza uhuru wa vyombo vya habari. Kwa Afrika Mashariki Tanzania ni nchi ya kwanza kwa uhuru wa vyombo vya habari. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa matokeo ya utafiti huu ni kwamba tunafanya vizuri. Utafiti huu inafuta dhana inayojaribu kujengwa kwamba nchi yetu inabinya na kuua uhuru wa vyombo vya habari. Hii ni taarifa ambayo imetokana na utafiti si suala la kubuni, ni utafiti umefanyika na taarifa hii imetolewa na iko hadharani na baadhi ya vyombo vya habari katika nchi yetu vimeripoti hii taarifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, imetokea dhana hapa…
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Na inajengwa kuonyesha kwamba…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waitara naomba ukae, Mheshimiwa Nape endelea.
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuonesha kwamba kuna mwingiliano mkubwa kati ya Serikali na mhimili wa Bunge. Baadhi ya wachangiaji wamefikia mahali pa kutoa hoja wakisema studio ya Bunge inaendeshwa na TBC.
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Na kwamba TBC wamevaa koti la Bunge na ndiyo wanaoendesha studio.
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni huu ufuatao. Studio ya Bunge inaendeshwa na Bunge na inasimamiwa na Bunge lenyewe. Walichofanya studio ya Bunge wameomba msaada wa kitaalamu (technical support) kutoka TBC.
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Na sisi Serikali kupitia TBC tumewasaidia kuwapa wataalam hao mpaka hapo watakapofika mahali wakaajiri wataalamu wao.
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Kusimama hapa Bungeni na kujaribu kuudanganya umma kwamba studio hii inaendeshwa na TBC maana yake Serikali imeingiza mikono ndani ya Bunge ni uongo wa mchana kweupe. Tunao wafanyakazi wa TBC ndiyo lakini pia wako wafanyakazi waliotoka taasisi zingine ambao Bunge kama taasisi huru inao uwezo wa kuazima wafanyakazi kutoka taasisi zingine kusaidia kutimiza wajibu wake. Hili siyo jambo baya wala siyo jambo geni, nilidhani hili niliweke sawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu na la mwisho. Iko hoja inazungumzwa kwamba matangazo yanayorushwa kutokea hapa…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Nape sekunde tatu…
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Sekunde tatu, basi naomba niunge mkono hoja.