Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Maulid Said Abdallah Mtulia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii na mimi kuchangia. Nashukuru kwa michango mizuri iliyotolewa na wenzangu, lakini na wawakilishi wetu wa Kambi Rasmi ya Upinzani na hasa kuonesha tofauti kwa sababu mara nyingi watu wengi wanafikiri upinzani ni kupinga tu, lakini leo upinzani umeonesha kabisa siyo lengo letu kupinga tu, mambo mazuri tunayaunga mkono. Kwa hiyo, hili nashukuru sana. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, na mimi naunga mkono hizi itifaki, lakini nina maeneo ambayo nayaona lazima tuyaangalie na tuyarekebishe.

Mheshikiwa Mwenyekiti, eneo la kwanza, Wajumbe wa Kamati na hata watu wa Kambi Rasmi ya Upinzani wamelalamikia suala la muda, kwamba wakati mwingine Serikali inaingia itifaki muda mrefu takribani miaka sita, bado hawajaleta Bungeni kwa ajili ya kuridhia hilo Azimio. Hili siyo jambo zuri. Naiomba Serikali itambue kwamba, Wabunge kwa ujumla wao wapo kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu. Tutajitajhidi kufanya lolote lile kwa maslahi ya nchi yetu, kwa hiyo, hata jambo lolote wakiliona zuri wasihofie wala tusiviziane, walete Bungeni na Wabunge huku kama kawaida yetu tutalichangia vizuri.

Kwa hiyo, hili jambo liangaliwe isiwe kawaida ya Serikali kuwa na wasiwasi wa kuleta jambo, jambo lolote lenye maslahi mapana ya nchi yetu wasiwe na kigugumizi, walilete tutalichangia, penye kasoro tutawaeleza, penye kuunga mkono tutaunga mkono, tuwe na utamaduni huo. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, wewe unajua sisi tuko Dar es Salaam pale, tunapozungumzia itifaki ya mambo haya ya bahari mimi nakubaliana na itifaki, lakini nina mashaka na utekelezaji wetu wa kazi zetu wenyewe.

Mheshimiwa Mwneyekiti, wewe Jimbo lako la Ilala pamoja na Jimbo langu mimi la Kinondoni tunaungana pale Salender Bridge, tuna mikoko na Serikali tunayo pale Dar es Salaam. Wizara ya Mazingira iko pale Dar es Salaam, lakini mikoko yetu inakufa pale Jangwani na maeneo mengine yote! Sasa haya yataondoshwa kwa itifaki haya? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua kwamba, tuna mto wetu pale Msimbazi, tuna Mto Ng’ombe na mito mingine, inaleta uharibifu mkubwa wa mafuriko ni kwa sababu tu ile mito hatuiangalii. Kwa taarifa tu mwaka huu Jangwani pale tumepita salama sana, nilitumia pesa zangu za Mfuko wa Jimbo kusafisha Mto na hatimaye mafuriko mwaka huu Jangwani pale hayakutokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hatuna utaratibu wa kulinda mito yetu hii, hizi itifaki sidhani kama zitatusaidia sana. Ni vizuri sasa kama Serikali yetu, kama Viongozi, tujikite katika kutatua matatizo yetu wenyewe, hizi itifaki ni jumla tu, itifaki haiwezi kuja kutuondolea matatizo yetu ya ndani ambayo sisi wenyewe hatufanyi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeweka sheria ya mita 60, hivi hii sheria ya mita 60 kuiacha bahari, hii bahari anaisafisha nani? Tunapokaa umbali wa mita 60 anayetegemewa sasa Serikali ndio ikafanye kazi za kusafisha mito. Je, inafanya? Tunapokaa umbali wa mita 60 inategemewa sasa bahari yetu Serikali ndio ikasafishe, matokeo yake bahari yetu inanuka. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, lakini ukienda nchi zilizoendelea, Paris hata ukienda Dubai, watu sasa hivi wanajenga mpaka kwenye bahari. Hizi sheria sisi tunaangalia kulingana na hali ya sasa au sheria tunaleta tu ili mradi? Lazima tutoe sheria ambazo zitaendana na wakati. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, watu wetu waruhusiwe kujenga kwenye bahari kwa lengo la kutunza hiyo bahari yenyewe. Watu wetu waruhusiwe kukaa karibu na mito kwa lengo la kutunza hiyo mito yenyewe, kwa sababu hiyo Serikali inayotaka watu wakae mbali, wao hawawezi kwenda huko wala hawawezi kwenda kutunza, badala yake tunakuwa na fukwe chafu, tunakuwa na mito michafu ni kwa sababu ya kutengeneza sheria ambazo wakati mwingine hatuna uwezo wa kwenda kuzisimamia. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, mfano watu wangu wa mabondeni pale wanatakiwa wahame, hivi pale Jangwani mtu anahama vipi wakati watu Dubai wanakaa baharini? Wewe unamhamishaje mtu Jangwani! Una mhamisha mtu Jangwani akakae Mabwepande wakati Jangwani anaenda Posta hata Kariakoo kwa mguu, Mabwepande anatumia nauli shilingi 2,000 na anatumia saa matatu! Mimi nafikiri hii siyo sawa, tutoke huko tuende katika ulimwengu wa kisasa. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, pale Dar es Salaam, Jangwani, watu wako wana uwezo wa kuendelea kukaa pale hakuna madhara yoyote. Ahsante.