Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshikiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nikazie pale alipoishia Mheshimiwa Msigwa na Waheshimiwa Wabunge wa Chama cha Mapinduzi niwaombe sana, hili Bunge ndiyo think tank ya nchi. Demand yetu ya kupata nyaraka muhimu kwa ajili ya kuishauri Serikali ni kwa sababu ya kutoa opinion ambazo zitawasaidia ninyi na Taifa letu na watoto wa watoto wetu. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, opinion zetu kila mara zinaonekana ni uadui, na hii ndiyo inasababisha kuanza kususiana futari, hii ndiyo inasababisha uhasama unakuwa ni uhasama. Kwa sababu hakuna opinion yetu ya msingi ambayo ninyi mtaichukua kama ni jambo muhimu katika Taifa hili. Sisi sote ni Watanzania, mnapokuja na hizi nyaraka sasa hivi naongea hapa hakuna hata hiyo hotuba ya Kambi ya Upinzani haipo mezani. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, leo tu asubuhi hapa tumeambiwa tutajadili habari ya Mikataba na Sheria za Madini mpaka Jumatano mwisho. Sheria hizo mnaleta kwa Hati ya Dharura. Wabunge wamekaa hapa miezi mitatu, wamechoka. Binadamu anapochoka ana-loose capacity ya ku-focus, leo tunaenda emotionally. Kwa sababu makinikia na ripoti zimesomwa mbili kwa Rais, television mkapeleka nchi nzima kwenye masoko waone, sasa leo mnataka ku- implement jambo hilo ndani ya siku nne, kinachotokea ni nini? Kitakachotokea mtafanya makosa yale mliyoyafanya kipindi cha mwanzo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi ndiyo Serikali, haya mambo kama yana umuhimu kwa kiwango hiki wapeni Wabunge hizi nyaraka wazisome, wapeni Wabunge hizi nyaraka wazipitie. Sasa kazi ya Mheshimiwa Jenista Mhagama hapa yeye, iko siku atatokea mtu huku aseme amegundua dawa ya UKIMWI, Mheshimiwa Jenista utasimama uombe utaratibu na ukatae kabisa, kama hiyo itakuwa inatibu kwa sababu haiwezekani kila opinion yetu mnaikataa, tunasema hakuna nyaraka mnakataa, tunawaambia hivi mnakataa, sasa tuishauri, futeni basi upinzani tubaki chama kimoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipindi kile CCM mko peke yenu kulikuwa kuna G7 tukiwa wadogo, mlikuwa mnashindana lakini mlikuwa hambaguani, sasa hivi tunaanza kupishana na tunaanza kubaguana. Narudia tena hiki mnachoendelea kupanda kitatoka hapo nje ya Bunge, kitakwenda mitaani. Haya yanayotokea Kibiti msishangae siku moja yakasambaa nchi nzima kwa sababu ya chuki zinazojengwa ndani ya Bunge hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya Mbunge ni kutoa ushauri sasa nitoe ushauri gani zaidi ya huu? Huu ndiyo ushauri, nasema hizi chuki mnazojenga ndani ya Bunge ndiyo zitatoka hapo nje, zikitoka hapo nje zitakwenda mitaani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia tena itafika mahali nchi hii itakuwa ni sehemu mbaya ya kuishi kwa sababu ninyi mlio wengi mmekataa kuchukua opinion zetu za msingi kwa sababu tu tumeitwa Wapinzani, utafikiri tumetoka Sudan sasa leo tunajadili mambo ya itifaki. (Makofi)

Haya mambo ya mazingira, DC wa Hai alikwenda akavunja vunja shamba la Mheshimiwa Mbowe, Sea Cliff Hotel na Golden Tulip ziko baharini sasa kwa sababu issue hapa ni itifaki ya kuridhia mazingira bora ya bahari na hizi hoteli basi zilizopo kando kando ya bahari zipigwe marufuku kabisa, ziwe mita 120 kutoka ufukwe wa bahari, kwa sababu issue kama leo ni itifaki ya mazingira ya bahari ambayo leo mmeilete hapa, ipi ilikuwa ni muhimu? Kwenda kuvunja shamba la mboga ama kuondoa Sea Cliff iliyoko pale kando kando ya bahari ambapo vichungi vya sigara vinatumbukizwa mle ndani? (Makofi)

Kwa hiyo haya mambo ya itifaki nilikuwa nataka tu niwaambie tu hichi ninachowaambia hivi mnavyoishi endeleeni, ila nawaaambia iko siku kama ambavyo sasa hivi hata issue za Kibiti mnaogopa kuzijadili utafikiri hamna kitu kinachiendelea. Kila mtu anaogopa kujadili humu ndani, Waziri wa Mambo ya Ndani naye anaogopa, nani anaogopa, Usalama wanaogopa kwa sababu mkianza kujadili tu ni kwamba jamaa wanaweza wakaja na hii inasababishwa na hasira ya wananchi. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba sana hasira hizi ambazo mnawapandikizia wananchi, mambo haya mnayotufanyia humu ndani ya Bunge, mnatuzuia tusiseme, mnatuzuia tusitoe opinion zetu, ninawashauri vunjeni siasa za vyama vingi katika Taifa hili mbaki wenyewe na familia zenu na wajukuu zenu.