Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mkataba mmoja pamoja na Itifaki mbili na nimepata wasaa wa kuzisoma soma hapa, lakini kwa kuwa kuna dakika tano nitajielekeza kwenye mambo machache tu.

Mheshimiwa Msigwa aliposema Bunge dhaifu husababisha Serikali dhaifu amenikumbusha kauli ambayo niliisema Bungeni hapa tarehe 19 mwaka 2012. Na kinyume chake, Serikali dhaifu vilevile husababisha Bunge kuwa dhaifu na ndiyo hali ambayo tunayo hivi sasa. Bunge letu limefanywa dhaifu sana na limefanywa dhaifu na Serikali na Serikali hii ingekuwa na nguvu ingejiamini sana, isingefanya Bunge kuwa dhaifu, lakini kwa sababu Serikali ni dhaifu ni lazima na Bunge nalo liwe dhaifu.

T A A R I F A . . . . .

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namwombea Mwenyenzi Mungu Mheshimiwa Mlinga aweze kubadilika hiyo tabia yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge hili limekuwa dhaifu kwa kiwango ambacho miswada, mkataba mmoja na Itifaki mbili zinaletwa zote kwa siku moja wakati ambapo Bunge lenye nguvu lingesema kwamba siku hii tunajadili mkataba huu, tunaujadili vizuri vinatafakari hoja umetolewa. Siku hii tunajadili mkataba huu, siku hii tunajadili mkataba huu. Kwa udhaifu huu wa Bunge unaoendelea anasema sikuwepo siku nyingi. Hii siku nyingine sikuwepo si Mwenyekiti unajua mlinitoa ndiyo maana sikuwepo. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya udhaifu huu Wabunge Mheshimiwa Halima Mdee hatakuwepo kwa muda wote ambao hatakuwepo, akija kurudi mtamwambia maneno haya haya. Mheshimiwa Ester Bulaya hatakuwepo hakirudi mtamwambia maneno haya haya. Sasa hii hoja ya uchafunzi wa mazingira upande wa bahari nizungumzie kwa niaba ya Mheshimiwa Mdee wa Jimbo la Kawe ambaye bahari inazunguka eneo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikataba hii Serikali iliisaini muda mrefu, lakini hakuna kinachofanyika kuzuia uchafuzi, hakuna kinachofanyika cha kutosha kunufaisha wavuvi. Nataka kusema nini hapa, kuridhia mikataba hii peke yake na Kambi ya Upinzani hapa inairidhia inaunga mkono kuridhiwa kwa hii mikataba haitoshi kama mwisho wa siku masharti ya msingi yaliyoko kwenye Itifaki, masharti ya msingi yaliyoko kwenye mikataba hayatekelezwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tutaruhusu Serikali kuendelea kuwa dhaifu na Bunge kuendelea kuwa dhaifu ni wazi siku zote tutapitisha mikataba na sheria lakini utekelezaji hakuna. Tuna Mkataba muhimu sana hapa, huu mkataba unahusu rasilimali za kijenetiki ambao nchi iliuingia mwaka 2010 tumeletewa leo kuridhia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matajiri unaowakuta duniani iwe ni akina Bill Gates, iwe ni tajiri wa Apple aliyefariki matajiri mnawakuta duniani walipata utajiri kwa sababu ya ubunifu. Wenzetu wana ubunifu wa kiteknolojia sisi tunawabunifu wengi sana ambao wangeweza kunufaika na rasilimali za kijenetiki kwenye ugunduzi wa dawa, tiba, vitu na mbalimbali lakini kwa sababu mambo haya hatuyafanyi vile inavyostahili ndiyo maana hatufiki pale ambazo tunafika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tumeingia katika sekta ambayo wengine ndiyo tunadhani ina manufaa zaidi ya madini. Kumbe huku kuna madini kwenye jenetiki, lakini hatufanyi ipasavyo. Hata kwenye madini tumewaambia muda mrefu leteni mikataba hapa Bungeni tumewaambia muda mrefu leteni mikataba leteni mikataba, tumeimba kwa miaka mingi leteni mikataba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mnatuletea hoja mnasema kwamba tunaleta sheria ya kulipa Bunge mamlaka juu ya mikataba halafu mnataka propaganda kama vile sisi ambao ndiyo tulikuwa tunasema mikataba iletwe tunakataa, sisi tunachokataa ni kwamba ninyi wa kuzileta sheria kwa Hati ya Dharura mnatunga sheria mbovu ambazo mwisho wa siku hazileti tija ambayo inasukudiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kweli ninyi mnataka kuisaidia nchi kwenye masuala ya madini, hata kama tukianzia na hapo ambapo nilisema Rais angekuwa makini asingeanzia na makinikia angeanzia na madini. Hata kama tukiamua kuanzia na makinikia cha kwanza ambacho Bunge ingetaka kwenye Bunge hili kabla hata kuletewa miswada kusoma kwa mara ya kwanza zile ripoti mbili zile, zile ripoti alizokabidhiwa Mheshimiwa Rais, ipaswa ziwasilishwe hapa Bungeni Mawaziri wazisome tuzijadili Wabunge halafu tuseme sasa Serikali kaandae mapendekezo ya muswada ya kuhusu hiki, kuhusu hiki, kuhusu hiki, iletwe hapa Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nachotaka kusema hapa ni kuwa, badala ya kuanza kujadili Miswada ya Sheria kwa Hati ya Dharura, Bunge hili liletewe kwa udharura huo huo ripoti mbili za Rais kuhusu makinikia, zisomwe hapa Bungeni, zijadiliwe hapa Bunge msipofanya hivyo ile kauli niliyosema kwamba Rais makini alipaswa kuanza na madini kabla ya makinikia kuna siku itakuja kuwatafuna.

Mheshimiwa Lema amesema kwamba kama hamtasikia maoni yetu basi ni afadhali mfike hatua mfute Kambi ya Upinzani. Mheshimiwa Lema kabla hawajafuta Kambi ya Upinzani kama wataendelea kutosikiliza maoni yetu imefikia hatua Watanzania waiondoe hii Serikali madarakani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mnadhani tumechelewa, kama mnashindwa tu kuwadhibiti wale watu wa Kibiti, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, kama mnashindwa kuwadhibiti watu wa Kibiti wanaotumia silaha, ndugu zangu hamuwezi kuwadhibiti Watanzania hawa wakiamua kutumia silaha yao, kadi yao kupigia kura kwenye sanduku la kura. (Makofi)