Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa fursa na niwashukuru Wabunge wote kwa umoja wao kwa kuridhia mapendekezo haya ya maazimio pamoja na itifaki tuliyoweka mezani. Kwa kuwa wameridhia kama ulivyosema sitakuwa na mengi ya kusema, niseme mawali tu ambayo yameleta sura za tofauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, Serikali strong, yenye nguvu ni Serikali inayochukua hatua, inatenda na siyo Serikali inayosema na hiki ndicho kinachoendelea. Mheshimiwa Mnyika anaposema tumeongea sana kwenye mikataba na anajua ukubwa wa mambo yale, lakini Serikali jasiri na yenye nguvu imeenda kwenye kutenda, hicho ndicho ambacho Wabunge na Watanzania wote wametamani muda mwingi sana kukiona na ndicho ambacho Mheshimiwa Rais anakwenda kukitenda na analiomba Bunge lione umuhimu huo kwa ukubwa wa rasilimali za nchi yetu na ukubwa wa jambo lenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ukigeugeu ndiyo ambao huwa unaweka mashaka kwamba mtu ambaye ameliongea kwa muda mrefu sana jambo, linapoletwa anageuka inaleta maswali kwamba huyu mtu amegeukaje. Nimemshukuru sana ndugu zangu hapa walipokuja kuongelea kwamba siyo kila kitu kupinga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili jambo ambalo lina maslahi ya Taifa, niwaambie Waheshimiwa Wabunge hata kama ataunga mkono mtu mmoja tu, Serikali hatuwezi tukarudi nyuma maadam tumepewa dhamana ya rasilimali za nchi yetu. Wabunge na kama Serikali na Wasaidizi wa Rais tunawahakikishia kwamba nia na dira aliyonayo Rais ni njema sana kwenye rasilimali za nchi yetu. Nawaombeni twende tuunge mkono wala tusipepesuke kwa kuzingatia vitu vingine ambavyo haviko kwenye dira yetu visije vikatutoa kwenye dira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengi sana ambayo yamo kwenye itifaki hizi yalishaletwa mbele ya Wabunge na Wabunge wameshafuatilia na yamefanyiwa kazi na watalaam ambao wana dhamana na wenyewe kwenye Taifa letu, hatuna haja ya kuwa na mashaka, niwaombe tuende turidhie ili yaweze kwenda kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengine Waheshimiwa Wabunge tunapoongelea ameongea Mheshimiwa Lema na Mheshimiwa Mnyika, ni vema sana tukawa makini sana tunapoongea. Nimemsikia akiongelea suala la Kibiti, lakini ningekuwa nakuuliza maswali mengi, najua usingepata majibu yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, kama una uhusiano na wale wahalifu hata ukadhani wameshinda, hebu waulize walianza wangapi na sasa wapo wangapi. Mwenzio Lema kwa sababu alikuwa kule gerezani anaweza akawaona wengine kule, wewe Mheshimiwa Mnyika ambaye hujaenda unaweza ukatusaidia, wewe unayedhani wameshinda wapo wangapi na wapo wapi? Lakini nikuhakikishie kwamba sisi kama Serikali hatutaacha eneo hata moja la nchi yetu hii likatawaliwa na uhalifu. Tutashughulika na mmoja mmoja na lazima haki ya watu wetu itasimama katika eneo lote la nchi yetu watasimama wakiwa wanafanya kazi kwa mazingira yaliyo salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaongea kimzaha mzaha, lakini taswira iliyopo ndani kabisa na niliisema mahali pengine, ina taswira hiyo ya siasa siasa. Leo hii ukituambia kwamba yale yanayoendelea Kibiti yataenda na maeneo mengine, tunaendelea tu kutafuta connection unajuaje kwamba yanaendelea na maeneo mengine. Kwa sababu kama anauawa Mwenyekiti wa CCM, anauawa wa CCM, wanaruka nyumba ya yule asiye wa CCM na wewe unasema yataendelea na maeneo mengine, una haja ya kutusaidia kujua kwa nini yataendelea na maeneo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini unadhani kwamba wanashinda,kwa sababu sisi kwenye mpango kazi wetu tuliopanga, tunaenda hatua kwa hatua kuhakikisha kwamba wananchi wa maeneo yote ya nchi yetu wanakuwa katika mazingira salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sentensi kama hizi pamoja na kwamba zimesemewa Bungeni nadhani kuna umuhimu sana ndugu zetu hawa watasaidia kujua kwamba kumbe sisi tunavyotafuta sana kumbe kiini ama kinatoka Bungeni au Serikalini, lakini sasa wanaenda kuhangaika na wananchi ambao ni very innocent, ndiyo maana sisi tunakuwa very responsible.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kwa sababu kwenye mambo ya siasa tunatakiwa tupambane sisi wanasiasa na siyo wananchi wengine ambao wanashughulika na shughuli zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa muda umeisha, ninaomba tu kutoa hoja kwamba Bunge lako sasa katika Mkutano wake wa Saba liridhie Maazimio tuliyoyaleta pamoja na marekebisho na Itifaki tuliyoleta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.