Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kazi za Ubaharia wa Shirika la Kazi Duniani na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Vitambulisho vya Mabaharia Na. 185 wa Mwaka 2003 wa Shirika la Kazi Duniani

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kazi za Ubaharia wa Shirika la Kazi Duniani na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Vitambulisho vya Mabaharia Na. 185 wa Mwaka 2003 wa Shirika la Kazi Duniani

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru. Nami niungane na waliotangulia kusema Wizara imefanya vizuri kuleta mikataba hii ili iweze kuridhia sasa kwa kuwa imechelewa kufanya hivyo kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunahitaji sasa kuwa na uangalifu wa hali ya juu kwamba lengo la kuridhiwa kwa mikataba hii ni kupunguza wimbi la uharamia huko baharini hasa bahari kuu. Sasa tunapokwenda kutoa vitambulisho kwa ajili ya kuwatambua wavuvi wetu tunahitaji kuwa na umakini wa hali ya juu sana kwa sababu vinginevyo wahalifu kutoka Mataifa mengine watajipenyeza na wao wapate vitambulisho hivi kutoka nchini kwetu ili waende kuvitumia vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, hatupaswi kuweka urasimu mkubwa ambao utawafanya sasa wavuvi wetu kwa maana ya Watanzania ambao wanastahili kupata vitambulisho hivi waanze kupata usumbufu mkubwa wa kuvipata, ni lazima tutengeneze utaratibu mzuri ambao hautakuwa na usumbufu ili wavuvi wetu waweze kuvipata vitambulisho ili waweze kufanya kazi zao vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuridhia ni jambo moja, tunahitaji pia sasa iletwe sheria ambayo tuje tuipitishe hapa kwa ajili ya utekelezaji wa mikataba hii. Kwa sababu kama tutairidhia leo, lakini sheria ya kusimamia utekelezaji wake na wenyewe utachukua miaka 10 bado tutakuwa hatujaenda kumaliza tatizo, Kwa hiyo, niishauri Serikali ifanye hivi kwa wakati.